Ticker

6/recent/ticker-posts

TUSIPOIFUNGA MANCHESTER UNITED,TUTAKUWA TUMEFANYA MAKOSA MAKUBWA :GUARDIOLA

Mhariri:Herman kihwili,IMEWEKWA.APR. 09,2014 SAA 12:08 JIONI
Pep Guardiola  ana amini kuwa itakuwa 'makosa makubwa ' kama Bayern Munich watashindwa kufikia hatua ya nusu
fainali ya  Ligi ya Mabingwa  kwa kuifunga Manchester United.

Bayern walitoka sare ya 1-1 katika uwanja wa Old Trafford katika robo-fainali ya kwanza , watakuwa bila mfungaji wao wa wiki iliyopita Bastian Schweinsteiger,pamoja na Javi Martinez na Thiago Alcantara.

Guardiola ana jaribu kuiga mtindo wa mtangulizi wake Jupp Heynckes, ambaye alishinda Bundesliga, Kikombe cha Ujerumani na Ligi ya Mabingwa msimu uliopita.

Kocha huyo wa zamani wa Barcelona Guardiola anafahamu ugumu wa kushinda taji la tatu tena na  ameamua kuwa kimya kimya katika uwanja wa  Allianz Arena siku ya leo Jumatano usiku.

"Hapa tunapambana," alisema Guardiola. "Mimi sipo hapa kwa kujinganisha mimi na Jupp alivyofanya msimu uliopita".

"Tumeshindi Bundesliga, na kama sisi hatutaingia katika  nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa ni makosa makubwa kwetu"

Post a Comment

0 Comments