Mhariri:Herman Kihwili. IMEWEKWA.OCT.6,2016 SAA 12:47 JIONI
Mambo makubwa yaliyojili hii leo katika mkutano wa waandishi wa Habari wa klabu ya Simba ni pamoja na kutangaza kamati mpya ya
mashindano.ambayo
tayari imeshaanza kazi rasmi.
Ofisa habari wa klabu iyo Haji Manara amesema wanaamini
kamati hiyo itaweza kufanikisha shughuli zote za mashindano ambazo klabu
itashiriki msimu huu.
Klabu ya Simba pia hii leo kupitia kwa Rais wa klabu hiyo Evans Aveva ,kamati ya
utendaji,sekretaliet,bechi la ufundi, wanachama na mashabiki wa klabu
hiyo,wamemuomba radhi rais magufuli kupitia kwa waziri nape, kwa kitendo kisicho
cha kiuungwana cha mashabiki wake kuvunja viti uwanjani .
Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Nape Moses Nnauye alitangaza kuvipiga marufuku klabu za Simba na Yanga kutumia uwanja wa Taifa kwa muda usiojulikana.
Waziri Nape alitangaza kuchukuwa uamuzi
huo baada ya kutembelea uwanja wa Taifa na
kubaini uharibifu mkubwa unaosemekana kufanywa na mashabiki wa Simba
waliong'oa Viti katika uwanja wa Taifa wakati wa mechi ya watani hao
wa jadi mchezo uliopigwa October 1 na kumalizika kwa sare ya 1-1.
Takribani Viti 1,781 vilivyokuwa katika jukwaa la klabu ya Simba Vimeng'olewa siku ya jana katika mchezo huo
Simba wamemuandikia barua rais magufuli ya kuomba radhi,
Simba wamesema endapo watabaini kama waliofanya uhalifu huo
ni wanachama wao basi watachukuwa hatua za kinidhabu kwa wanachama hao,huku
klabu hiyo ikiaamini rais atawaruhusu kutumia tena uwanja wa taifa kwa kuwa ni waelewa.
Katika Hatua nyingine Klabu ya Simba pia kupitia kwa msemaji wao Haji Manara
wametoa ombi kwa bodi ya ligi na Tff kuhakikisha wanachagua waamuzi sahihi wa
kuchezesha mechi kubwa.
Simba wamesema wapo tayari kugharamia malipo ya waamuzi kutoka nje
ya Nchi kuchezesha mechi zao kama ikibidi swala hilo.

0 Comments