Ticker

6/recent/ticker-posts

PICHA: YANGA YAIANGAMIZA MTIBWA,CHIRWA AFUNGUA AKAUNTI YA MABAO

Mhariri:Herman Kihwili. IMEWEKWA.OCT.12,2016 SAA 02:00 USIKU
Klabu ya Yanga Hii leo imeibuka na ushindi mzito wa mabao 3-1 dhidi ya Mtibwa Sugar ya Morogoro katika mchezo wa Ligi Kuu ya
Vodacom Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Ushindi huo umerejesha matumaini kwa mabingwa watetezi hao wa Ligi kuu Tanzania Bara
.
Hadi mapumziko, Yanga walikuwa mbele kwa bao 1-0 lililofungwa na winga Mzambia, Obrey Chirwa dakika chache kabla ya kwenda mapumziko.
Obrey Chilwa akishangilia bao lake la kwanza kwa Yanga tangu asajiliwe

Yanga walifanikiwa kupata bao la pili dakika ya 68 kupitia kwa Msuva kabla ya mshambuliaji aliyetokea benchi Donald Ngoma kufunga la tatu dakika ya 80 akimalizia pasi nzuri ya Mwashiuya.

Yanga ililazimika kumalizia pungufu baada ya mshambuliaji Amissi Tambwe kutolewa nje baada ya kugongana na Shaaban Nditi na kupasuka kwenye dakika ya 87.

Kikosi cha Mtibwa

Kikosi cha Yanga

Yanga sasa imefikisha pointi 14 baada ya kucheza mechi saba, inazidiwa pointi sita na mahasimu wao wa jadi, Simba SC walio kileleni ingawa wamecheza mechi moja zaidi.


ANGALIA PICHA











KWA TAARIFA,BREAKING NEWS,RATIBA PAMOJA NA MATOKEO YA MECHI MBALIMBALI,LIKE PAGE YA FACEBOOK  BONYEZA HAPA (Jamii na Michezo)

Post a Comment

0 Comments