Ticker

6/recent/ticker-posts

LIGI YA MABINGWA:LAURENT BLANC ASEMA WANAHITAJI KUISHAMBULIA CHELSEA

Mhariri:Herman kihwili,IMEWEKWA.APR. 08,2014 SAA 11:46 JIONI
Kocha wa Paris St Germain Laurent Blanc anataka timu yake kutumia mfumo wa kushambulia dhidi ya Chelsea katika mchezo
wao wa  Ligi ya Mabingwa hatua robo fainali ya pili katika uwanja wa Stamford Bridge siku ya leo Jumanne licha ya kuwa na fahari ya faida mabao mawili.

PSG, ambao walishinda michezo 11 mfululizo katika mashindano yote, wanajivunia kuongoza kwa  3-1 katika mechi ya kwanza iliyopigwa katika uwanja wa Parc des Princes wiki iliyopita.

Baada ya kupoteza mchezo wao mmoja tu kati ya 17 ya michezo ya Ligi ya Mabingwa , Blanc ana ujasiri timu yake itafika nusu fainali kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1995, lakini anatarajia kuwepo kwa hali ya kuzorota kutoka kwa timu ya Jose Mourinho. 

"Tunaamini baadhi ya mambo na mimi siku zote naamini kuwa tutakuwa na mchezo wa upinzani ambao utakuwa bora kwa kushinda kikombe," alisema Blanc.
 
"hatujaja hapa kuteseka na basi la Chelsea tutalazimisha mchezo wetu na kuutawala wote. Jukumu la timu iliyo juu ni kuutawala mchezo hata ukiwa mbali na nyumbani".
 
"Falsafa yetu ni moja ya kushambulia,ni kama kuweka mpira na kusababisha matatizo kama msimamo wetu. Itakuwa ajabu kujaribu kufaulu kwa kuiacha falsafa hii katika hatua moja ama nyingine."
 
Mshambuliaji wa Swedish  Zlatan Ibrahimovic, ambaye alifunga mabao 10 ya Ligi ya Mabingwa msimu huu, atakosa  mchezo huu baada ya kuumia mguu  katika mechi ya kwanza.
 
 

Post a Comment

0 Comments