Ticker

6/recent/ticker-posts

KIBARUA CHA DAVID MOYES KUOTA NYASI WAKATI WOWOTE KUANZIA SASA,WAMILIKI WA KLABU HIYO WAMCHOKA KUCHA HUYO

Mhariri:Herman kihwili,IMEWEKWA.APR. 21,2014 SAA 01:30 USIKU
David Moyes inakabiliwa na wakati mgunia wakuwa kama meneja wa Manchester United, kwa mujibu wa taarifa
zisizothibitishwa.

Mabingwa hao wa Ligi Kuu wanaomaliza muda wao wamekataa kutoa maoni juu ya taarifa nyingi za magazeti kadhaa ya kitaifa, kudai kuondoka kwa kocha huyo.

Moyes amekuwa na wakati mgumu mno tangu kuchukua kazi ya kukinoa kikosi cha United mwisho majira ya joto, lakini klabu walitarajiwa kuwa imara na Mscot huyo licha ya ukosefu wa mafanikio katika mashindano ya ndani na Ulaya.

Bodi ya United inaonekana kuweza kupunguza mkataba wa miaka sita wa Moyes ambaye hivi karibuni alifungwa mabao 2-0 na klabu yake ya zamani Everton, ambapo kwa sasa United wana pointi  13 nyuma ya timu inayoshikilia nafasi ya nne katika Ligi Kuu.

Kufika robo fainali ya Ligi ya Mabingwa UEFA kuliweza kupunguza pressure  juu ya Moyes, lakini wakatolewa nje kwa jumla ya mabao 4-2 dhidi ya Bayern Munich.

Sir Alex Ferguson alikuwa na wito kwa klabu hiyo ya kumchukuwa meneja huyo wakati alipoamua kustaafu mwezi Mei baada ya kung `aa na kuitumikia klabu hiyo ya Old Trafford, lakini wamiliki wa klabu hiyo ambao ni familia Glazer, wanaonekana kupoteza uvumilivu na kucha huyo.

Ferguson, ambaye huwa anaangalia michezo mingi ya United akiwa katika jukwaa, mwenyewe alikuwa mgumu kutumia pesa kwa kipindi chake cha miaka 27, lakini alishinda vikombe vya UEFA Ligi ya Mabingwa mara mbili, vikombe vya Ligi Kuu mara13  na na vikombe vitano vya FA.

United wanatarajiwa kutumia sana katika majira ya joto, na mrithi wa kocha huyo atakabidhiwa pesa za usajili , ambapo  taarifa zinasema ni karibu  na £ 150million.

Meneja wa Uholanzi Louis van Gaal, ambaye ataondoka baada ya Kombe la Dunia,bosi wa Borussia Dortmund Jurgen Klopp, na wa Paris St-Germain  Laurent Blanc wamekuwa wakipigiwa upatu kama wagombea ,na  inawezekana kuchukua nafasi ya Moyes.

Post a Comment

0 Comments