Ticker

6/recent/ticker-posts

BOSI WA TOTTENHAM TIM SHERWOOD AFAFANUA HASARA KWA GARETH BALE

Mhariri:Herman kihwili,IMEWEKWA.APR. 18,2014 SAA 09:21 ALFAJIRI
Tim Sherwood anaamini Tottenham ingeweza kuwa na changamoto
katika mbio za kupata taji la ligi kuu msimu huu kama bado Gareth Bale angekuwa katika timu yao.

Bale, 24, alikuwa mahiri kwa Spurs msimu uliopita, na alifunga mabao 26 katika mashindano yote, kabla ya kuuzwa katika majira ya joto kwenda Real Madrid kwa uhamisho ambao ni rekodi ya dunia kwa kiasi cha £ 85m.

Mchezaji huyo amekuwa vizuri kwa timu ya Hispania katika msimu huu, kwa kufunga mabao 20 katika mechi 38, ikiwa ni pamoja na goli alilotumia nguvu binafsi siku ya Jumatano usiku katika fainali ya Copa del Rey dhidi ya Barcelona. 

Tottenham, ambao pia walimuuzwa kiungo Luka Modric kwa Real Agosti 2012 kwa ada iliyoaminika kuwa ni karibu na £ 33m, timu hiyo inajitahidi ili kudumisha changamoto za kufuzu katika Ligi ya Mabingwa msimu ujao, sasa ni wa sita katika msimamo, pointi saba nyuma ya Arsenal walioko katika nafasi ya nne. 

Alipoulizwa kuhusu bao la Bale aliloshinda katika ushindi wa Real 2-1 dhidi ya Barca, Sherwood alijibu: "Hiyo ni biashara kwa kawaida kwa Gareth Bale". 

"Tuliona aliyoyafanya mwaka jana: mabao 21 na kusaidia mara tisa, alifunga mabao ya ushindi katika mechi nane". 

"Tunaweza kufanya kwa sasa, kwa njia yeyote. Kama tukichukuwa pointi zote na zitakazotuweka kuwa juu pengine tutakuwa katika changamoto za kugombea taji".

"Wachezaji wawili bora uwanjani jana usiku (katika fainali ya Copa del Rey ) walikuwa ni Gareth Bale na Luka Modric na nasema hivyo kwa kila kitu."

Spurs watakutana na  Fulham siku ya Jumamosi kwa lengo la kuziba pengo kati yao na timu iliyokuwa katika nafasi ya tano  Everton.

Sherwood alikiri kwamba ushiriki wa timu yake katika Europa Ligi msimu huu ulikuwa umeiweka timu yake katika mzigo mkubwa , lakini alikuwa na nia ya kuwaona vijana wake wakimaliza na  nguvu kama ingewezekana.

Post a Comment

0 Comments