Mhariri:Herman Kihwili. IMEWEKWA.OCT.2,2016 SAA 12:30 MCHANA
Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Nape Moses Nnauye ametangaza kupiga marufuku klabu za Simba na Yanga
kutumia uwanja wa Taifa kwa muda usiojulikana.Waziri Nape ametangaza kuchukuwa uamuzi huo mapema hii leo Hasubui mara baada ya kutembelea uwanja wa Taifa na kubaini uharibifu mkubwa unaosemekana kufanywa na mashabiki wa Simba waliong'oa Viti katika uwanja wa Taifa wakati wa mechi ya watani hao wa jadi mchezo uliopigwa hapo jana na kumalizika kwa sare ya 1-1.
![]() |
| Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Nape Moses Nnauye akikagua uhalibifu uliofanya hapo jana na mashabiki wanaosemekana kuwa ni wa Simba |
Takribani Viti 1,781 vilivyokuwa katika jukwaa la klabu ya Simba Vimeng'olewa siku ya jana katika mchezo huo
Nape pia amesema uhalibufu uliofanyika hapo jana Klabu husika zitalipa na watakamata mgao wao mpaka watapohakikisha kuwa wamelipa gharama zote.
Simba na Yanga hawatatumia uwanja wa Taifa kwa mechi na Timu yeyote ile,lakini wanaweza kutumia viwanja vingine kama Uhuru N.K





0 Comments