Ticker

6/recent/ticker-posts

PICHA:WAZIRI NAPE AZINDUA MFUMO WA TIKETI ZA KIELEKTRONIKI UWANJA WA TAIFA

 Mhariri:Herman Kihwili. IMEWEKWA.SEPT.11,2016 SAA 02:15 USIKU

Waziri wa habari Sanaa utamaduni na michezo Nape Nnauye hi leo amezindua mfumo matumizi ya Tiketi za kielectroniki katika
uwanja wa taifa jijii Dar es salaam.

Akizungumza katika uzinduzi huo Nape Nnauye amesema kuwa Mfumo huo kuwekwa katika kiwanja cha Taifa ni muendelezo wa serikali kuwekeza katika michezo na  kuhakikisha sekta ya michezo inasonga mbele.





Nape pia amewataka watanzania kujivunia mfumo huo kwani ni moja ya mifumo bora iliyowekwa katika viwanja kwa nchi za ukanda wa kusini mwa jangwa la sahara.

Nape pia amewataka watanzania kutambua kuwa kuwekwa kwa mfumo huo ni moja ya sehemu ya gharama za uwanja huo.

 kampuni ya Selcom ni kampuni ya kitanzania ndiyo iliyopewa dhamana ya kufunga mitambo hiyo ya tiketi za kielecteronini.


Kwa upande wa Shirikisho la soka nchini Tanzania TFF ambao ni wadau wakubwa wa uwanja huo,kwa kupitia rais wake Jamali Malinzi,ameiomba serikali kutumia mfumo huo kwa kuangalia Zaidi maslai ya  vilabu.

Sambamba na hilo Jamali malinzi ameelezea changamoto mbali mbali walizokutananazo kwa mara ya kwanza walipoutumia mfumfumo huo na kutoa wito kwa Serikali kuzifanyia kazi.


Kwa upande wa vilabu vya ligi kuu Tanzania Bara,Jamii na Michezo imezungumza na Katibu mkuu wa klabu ya Simba Patrick kahemelea ambaye wao wameupokea kwa moyo mkunjufu mfumo huo mfumo huo.

Kwa upande wa mchezo wa Netball ambapo viwanja vyao navyo vipo katika uwanja wa huo wa Taifa ,Jamii na michezo imezungumza na mwenyekiti wa chama cha mchezo huo Zainabu Mbilo,ambaye amesema kwa sasa wako katika mchakato wa kuhakikisha mchezo huo unapata udhamini ili wanapocheza katika uwanja huo,mchezo huo uwe pia na viingilio na kupata fedha za kuendeleza mchezo huo. 

ANGALIA PICHA









KWA TAARIFA,BREAKING NEWS,RATIBA PAMOJA NA MATOKEO YA MECHI MBALIMBALI,LIKE PAGE YA FACEBOOK  BONYEZA HAPA (Jamii na Michezo)


Post a Comment

0 Comments