Mhariri:Herman Kihwili. IMEWEKWA.SEPT.11,2016 SAA 02:36 USIKU
Klabu ya Simba imeendelea kujiimalisha katika Ligi kuu ya Soka Tanzania Bara baada ya
kuchomoka na ushindi wa
mabao 2-0 dhidi ya Mtibwa Sugar jioni ya leo jumapili katika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.
mabao 2-0 dhidi ya Mtibwa Sugar jioni ya leo jumapili katika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.
Mabao ya Simba hii leo yamefungwa na Ibrahim Hajib dakika ya 52 kwa kichwa akimalizia kona nzuri iliyochongwa na
beki Mohammed Hussein 'Tshabalala', pamoja na Laudit Mavugo dakika ya 66
akiwa ndani ya boksi baada ya pasi ya kiungo Mwinyi Kazimoto Mabao yote yamefungwa
kipindi cha pili.
Simba SC imefikisha alama 10 baada ya kucheza
mechi nne, wakishinda tatu na sare moja.
African Lyon ya Dar es Salaam kesho Septemba 12, 2016 itaikaribisha Mbao FC kwenye mchezo Mchezo huo Na. 28 wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara utakaofanyika Uwanja wa Uhuru jijini.
Mara baada ya mechi hiyo, raundi ya tano itafanyika mwishoni mwa wiki ijayo kadiri ya ratiba.
African Lyon ya Dar es Salaam kesho Septemba 12, 2016 itaikaribisha Mbao FC kwenye mchezo Mchezo huo Na. 28 wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara utakaofanyika Uwanja wa Uhuru jijini.
Mara baada ya mechi hiyo, raundi ya tano itafanyika mwishoni mwa wiki ijayo kadiri ya ratiba.
ANGALIA PICHA
0 Comments