Ticker

6/recent/ticker-posts

AZAM v SIMBA KUWAPISHA CONGO-BRAZZAVILLE, SASA KUPIGWA SEPTEMBA 21 UWANJA WA TAIFA

 Mhariri:Herman Kihwili. IMEWEKWA.SEPT.12,2016 SAA 01:35 USIKU

Mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) kati ya Azam FC na Simba ya Dar es Salaam, utafanyika Jumatano
Septemba 21, 2016 badala ya Septemba 17, mwaka huu.

Mchezo huo utakaofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, umesogezwa mbele kuipisha timu ya taifa ya Congo-Brazzaville ambao watacheza na Serengeti Boys,ili ipate nafasi ya kufanya mazoezi kwenye Uwanja wa Taifa, ikiwa ni kutekeleza matakwa ya kanuni za mchezo wa mpira wa miguu za kimataifa kwamba mwenyeji lazima aachie uwanja siku moja au saa 24 kabla ya mchezo wa ushindani.

KWA TAARIFA,BREAKING NEWS,RATIBA PAMOJA NA MATOKEO YA MECHI MBALIMBALI,LIKE PAGE YA FACEBOOK  BONYEZA HAPA (Jamii na Michezo)


Post a Comment

0 Comments