Ticker

6/recent/ticker-posts

HAMIS KIIZA KUFANYA VIPIMO VYA AFYA

Mhariri:Herman Kihwili. IMEWEKWA.JULY.01,2015 SAA 01:13 USIKU
Klabu ya Simba inaendelea na mkakati wa kuboresha timu kwa ajili ya msimu wa mwaka 2015 – 2016. Baada ya
kuboresha benchi la ufundi kwa kupata kocha mpya, kocha wa viungo na kocha wa magolikipa, Simba Sports Club imegeukia uboreshaji wa timu yake.
Katika zoezi hili tunapenda wanachama na wapenzi wa Simba mpate taarifa rasmi kuwa Hamis Kiiza atafika nchini siku ya Alhamisi tarehe 2 July 2015 kwa ajili ya kufanya vipimo. Ikiwa atafanikiwa vipimo basi utaratibu wa usajili utaendelea.
Hamis Kiiza ni mchezaji kutoka Uganda ambaye pia anacheza timu ya Taifa ya Uganda, Uganda Cranes.
KWA TAARIFA,BREAKING NEWS,RATIBA PAMOJA NA MATOKEO YA MECHI MBALIMBALI,LIKE PAGE YA FACEBOOK  BONYEZA HAPA (Jamii na Michezo)

Post a Comment

0 Comments