Aston Villa tayari wamemsajili mshambuliaji Jordan Ayew kutoka klabu ya Ufaransa Lorient.
Ayew anaungana wachezaji wenzake wa zamani wa Ligue 1 Jordan Amavi na Idrissa Gueye katika dimba la Villa Park, na mtoto huyo wa Abedi Pele,anaweza kujikuta anacheza dhidi ya ndugu Andre, ambaye amesaini katika klabu ya Swansea.
Andre na Jordan Ayew ni wachezaji wa timu ya taifa ya Ghana, Black Stars,na wamewahi pia kufundishwa na Kwesi Appiah ambaye sasa ni kocha wa timu ya Al Khartoum kutoka nchini Sudan,ambayo leo imeifunga APR ya Rwanda mabao 4 - 0 na kutinga hatua ya nusu fainali, ya michuano ya Vilabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kagame Cup 2015) .
Jordan Ayew ambaye ni Mshambuliaji wa zamani wa Marseille , alifunga mabao 12 katika mechi 26 za ligi akiwa na Lorient msimu uliopita na ameitwa mara 28 katika kikosi cha Ghana, atakuwa mbadala moja kwa moja wa Christian Benteke aliyehamia Liverpool kwa £ 32.5m.
"Najisikia radhi kwa kumleta Jordan katika klabu ," bosi wa Villa Tim Sherwood aliiambia tovuti rasmi ya klabu hiyo.
"Yeye ni mchezaji kijana mzuri ambaye kikamilifu anafaa kwa Ligi Kuu."Tim Sherwood alifafanua.
KWA TAARIFA,BREAKING NEWS,RATIBA PAMOJA NA MATOKEO YA MECHI MBALIMBALI,LIKE PAGE YA FACEBOOK BONYEZA HAPA (Jamii na Michezo)


0 Comments