Ticker

6/recent/ticker-posts

MASHABIKI WA MACHESTER CITY,WAWAPIGIA MAGOTI VIONGOZI WA MAN UNITED KUHUSU KUTIMUA MOYES

Mhariri:Herman kihwili,IMEWEKWA.APR. 22,2014 SAA 06:50 USIKU
Mashabiki wa Manchester City wamewasisitiza wapinzani wao Manchester United kuwa hawapaswi kumtimua meneja

wao David Moyes baada ya siku nzima kutawala uvumi wa kumfukuza kocha huyo.

Mocked: Manchester City fans hold up a banner in the stands which reads 'Don't Sack Moyes'
Vita vya panzi ni furaha kwa kunguru: mashabiki Manchester City wakishikilia bendera ya kumuombea David Muyes  ambayo inasomeka'Msimfungie virago  Moyes' (wakileta utani)
Having their say: 'David Moyes is a football genius', jokes another City fan
Kila mtu alikuwa na mawazo yake: 'David Moyes ni mtu wa Fikra ya soka', Shabiki wa City akileta utani 
Mashabiki hao walibeba mabango yaliyosomeka  ' Usimfukuze Moyes' na lingine  'David Moyes: Football Genius' wakati wa mchezo wao wa Ligi Kuu na West Bromwich Albion siku ya Jumatatu usiku.
Cross City: Fans displayed the messages before the Premier League clash with West Brom
Mashabiki  wa City wakionyeshwa ujumbe kabla ya mchezo wao wa  Ligi Kuu na West Brom
Inevitable: Moyes is to be sacked by Manchester United after a dismal first season in charge
Taarifa zimeripotiwa kuwa Moyes ataachishwa kazi ya kuwa na Manchester United baada ya matokeo mabaya ya msimu wa kwanza  wa malipo
Keeping faith: City were still in the title race before the game, but Liverpool are in pole position
Kuweka imani: City bado wako katika mbio za kutwaa ubingwa , lakini Liverpool wana  nafasi kubwa.

Vyombo vya habari nchini Uingereza vimeripoti kuwa Moyes atatimuliwa katika klabu ya Manchester United katika kipindi cha wiki zinazokuja baada ya wamiliki wa Klabu ya United ,familia Glazer  hatimaye wamepoteza uvumilivu na Mscot huyo ambaye aliteuliwa  msimu uliopita baada ya kustaafu kwa Sir Alex Ferguson,na sababu pekee ya kupoteza matumaini na kocha huyo ni kufuatia msururu wa matokeo mabaya msimu huu.

Lakini Klabu ya Manchester United inasema kuwa David Moyes hajafutwa kazi na kukataa kuzungumzia mstakabali wa kocha huyo katika klabu hiyo.

Msemaji wa klabu hiyo alithibitisha kuwa Moyes bado hajafutwa kazi.

Alipohojiwa kuhusu ikiwa kocha huyo ataaga klabu hiyo kabla ya mwisho wa msimu,alijibu kwa kusema kawaida hawazungumzii utabiri.

Hata hivyo hakuna hata gazeti moja lililosema moja kwa moja kuwa Moyes amefutwa kazi.

Jarida la Daily Mail limenukuliwa likisema kuwa Moyes huenda akafutwa kazi kabla ya msimu kuisha wakati Daily Telegraph likisema amepoteza uungwaji mkono wa wamiliki wa klabu hiyo na huenda akafutwa kazi.

Moyes aliteuliwa na Sir Alex Ferguson, kumrithi kama meneja wa klabu hiyo alipostaafu baada ya kuhudumu kama meneja kwa miaka 26

Moyes mwenye umri wa miaka 50, alipewa mkataba wa miaka sita na kuondoka Everton kuongoza mabingwa wa ligi lakini mkataba wake huenda unaelekea ukingoni baada tu ya miezi kumi.





Post a Comment

0 Comments