Ticker

6/recent/ticker-posts

MATOKEO KATIKA MICHEZO YA LIGI KUU TZ BARA NA RATIBA YA KESHO JUMAPILI

Mhariri:Herman Kihwili,IMEWEKWA March. 08,2014 SAA 01:49 USIKU
Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) imeendelea leo (Machi 8 mwaka huu) kwa mechi tatu ambapo Coastal Union waliumana na
Ashanti United kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.

Na katika mchezo huo wenyeji Coastal Union wameshindwa kufurukuta baada ya kulazimishwa sare ya bila kufungana.

Ruvu Shooting iliwakaribisha Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Mabatini, Mlandizi mkoani Pwania,na maafande hao wa Ruvu Shooting waliwachezesha gwaride maafande wenzao wa kuwafunga bao 1 kwa 0.

Na Mbeya City imeendeleza ubabe kwa kewatandika Rhino Rangers mabao 3 kwa 1,katika mchezo uliopigwa kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.

Mechi za kesho Jumapili (Machi 9 mwaka huu) ni Tanzania Prisons na Simba kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya, na JKT Ruvu na Mtibwa Sugar zitacheza Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi, Dar es Salaam.

Post a Comment

0 Comments