Ticker

6/recent/ticker-posts

UJIO WA SUPER MARIO BALOTELLI KATIKA KIKOSI CHA AC MILAN

Mhariri:Herman Kihwili,IMEWEKWA March. 08,2014 SAA 06:06  MCHANA

Mario Balotelli anarudi katika kikosi cha AC Milan kwa ajili ya mechi yao ya  Serie A dhidi ya Udinese siku ya leo Jumamosi baada
ya kupona kutokana na kuumia bega.

"Balotelli yuko vizuri, bado anajisikia maumivu kidogo lakini anahitaji ya mazoezi ili kuwa pamoja.,"Kocha wa  Milan Clarence Seedorf aliwaambia waandishi wa habari siku ya Ijumaa.

Mshambuliaji huyo wa Italia, ambaye amefunga mabao 10 katika mechi 18 msimu huu, amekosa mechi mbili za mwasho za  Milan baada ya kuondoka uwanja dakika 12 kutoka mwisho katika mchezo  wa Ligi ya Mabingwa ambao walifungwa 1-0 na Atletico Madrid mwezi uliopita. 

Mshambuliaji huyo amekuwa katika utata zaidi baada ya kuchapisha picha yeye mwenyewe katika ukurasa wake wa Twitter akicheza mchezo wa table tennis, hivyo kuzua madai katika vyombo vya habari  vya nchini Italia kwamba alikuwa hachukulii kwa umakini kuumia kwake.

"Siko hapa kwa ajili ya  kuwaambia watu jinsi ya kutumia njia za mawasiliano yao wenyewe," Seedorf alisema. 

"Ki vipi  unapata habari nchini Italia na kuwa na wasiwasi kwangu. Hili ni jambo kama lasilo na maana. Ni nani anayejali ikiwa alicheza table tennis? Alikuwa kwa saa sita kwa  matibabu." 

Vijana hao wa Seedorf wako katika nafasi ya  10 katika Serie A wakiwa na pointi 35, sita nyuma ya wapinzani wao wa jadi Inter Milan,Wao watasafiri kwenda katika mji mkuu wa Hispania siku ya Jumanne kwa raundi ya pili ya hatua ya-16 bora kupambana na Atletico.
 

Post a Comment

0 Comments