Mhariri:Herman kihwili,IMEWEKWA March. 25,2014 SAA 08:13 USIKU
Bosi wa Manchester City Manuel Pellegrini anasema ana
amini wanaweza wakatoka bila ushindi katika derby ya siku ya leo Jumanne dhidi ya Manchester United.
amini wanaweza wakatoka bila ushindi katika derby ya siku ya leo Jumanne dhidi ya Manchester United.
Vijana wa Pellegrini wanafaida ya alama 12 ,mbele ya wapinzani wao United na wanajua ushindi katika uwanja wa Old Trafford ni misaada mkubwa kwao kwa ajili kuchukuwa taji la pili la Ligi Kuu katika kipindi cha miaka mitatu.
Lakini kocha huyo wa Chile, ambao alionja ladha ya kwanza ya Manchester derby kwa kuifunga United mabao 4-1 katika Uwanja wa Etihad mwezi Septemba mwaka jana, watakuwa ugenini katika mchezo wa hii leo, huku akipendekeza kwamba nguvu ya ziada inahitajika ili kuwawezesha timu yake kufanya vizuri katika mchezo huo.
Pellegrini alisema: "sidhani kwamba sisi ni bora katika mchezo wowote,tuna wakati mzuri lakini sisi tunacheza dhidi ya timu kubwa katika uwanja wao wenyewe, hivyo sidhani sisi ni mabingwa".
"Bila shaka sisi daima tunatarajia kwenda na kushinda kila mchezo.lakini Narudia, kwa sababu tu Manchester United wako katika msimu mgumu, haina maana ya sisi tuna kwenda kushinda".
"Tuna kwenda huko na kucheza mchezo mzuri sana."
City wako nyuma kwa pointi sita dhidi ya viongozi wa Ligi Kuu Chelsea na wakiwa na michezo mitatu mkononi, na Pellegrini atakuwa na nahodha Vincent Kompany ili kuimarisha upande wake wa ulinzi katika uwanja wa Old Trafford.
United wanakwenda katika derby wakiwa katika roho nzuri kwa mafanikio mfululizo dhidi ya Olympiakos na West Ham, lakini Pellegrini pia anaamini timu yake iliyokuwa ikitafakari wiki ya mateso dhidi ya Wigan na Barcelona mapema mwezi huu, inaweza kusimama na kufanya vizuri zaidi .
0 Comments