IMEWEKWA FEB. 18,2014 SAA 01:13 USIKU
Shirikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limewalalamikia wana familia watano wa mpira
wa miguu kwa Kamati ya Maadili kuhusiana na udanganyifu katika
mtihani wa
utimamu wa mwili wa waamuzi na usajili wa mchezaji Emmanuel Okwi.
Riziki
Majala na Army Sentimea ambao ni wakufunzi wa waamuzi, na Oden Mbaga na Samwel
Mpenzu ambao ni waamuzi wanadaiwa kughushi nyaraka kuhalalisha mtihani huo kinyume
cha taratibu.
Naye
Sabri Mtulla analalamikiwa na TFF kwa madai ya kuidanganya Kamati ya Sheria na
Hadhi za Wachezaji kuwa hakukuwa na pingamizi lolote juu ya usajili wa mchezaji
Emmanuel Okwi huku akijua wazi kuwa jambo hilo si kweli.
Kwa
mujibu wa kanuni, malalamiko hayo yamefikishwa kwenye Kamati ya Maadili ambayo
itachunguza ili kujiridhisha kama yana msingi au la. Ikibaini kuna kesi ndipo
walalamikiwa watafika mbele ya kamati hiyo.
TWIGA STARS,
ZAMBIA KUCHEZA MACHI 2
Mechi
ya pili ya raundi ya kwanza kuwania Kombe la Afrika kwa Wanawake (AWC) kati ya
Tanzania (Twiga Stars) na Zambia (Shepolopolo) itachezwa Machi 2 mwaka huu
Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi, Dar es Salaam.
Twiga
Stars tayari imeingia kambini kujiandaa kwa mechi hiyo itakayochezwa kuanzia
saa 10 kamili jioni. Twiga Stars chini ya Kocha Rogasian Kaijage inafanya
mazoezi yake kwenye Uwanja wa Karume ambao ni wa nyasi za bandia kama ulivyo
ule wa Azam Complex.
Shepolopolo
iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 katika mechi ya kwanza iliyochezwa Februari 14
mwaka huu kwenye Uwanja wa Nkoloma jijini Lusaka.
Iwapo
Twiga Stars itafanikiwa kuiondoa Shepolopolo itacheza na mshindi wa mechi kati
ya Botswana na Zimbabwe. Zimbabwe ilishinda mechi ya kwanza ugenini.
Wachezaji
wa Twiga Stars waliopo kambini ni Amina
Ali, Anastazia Katunzi, Asha Rashid, Donisia Minja, Esther Chabruma, Etoe
Mlenzi, Everine Sekikubo, Fatuma Issa, Fatuma Makusanya, Fatuma Mustafa, Fatuma
Mwisendi, Fatuma Omari, Flora Kayanda, Happiness Mwaipaja, Maimuna Mkane, Mwajuma
Abdallah, Mwapewa Mtumwa, Pulkeria Charaji, Sherida Boniface, Sophia Mwasikili,
Therese Yona, Vumilia Maarifa na Zena Said.
0 Comments