Ticker

6/recent/ticker-posts

RAIS MALINZI AENDA KUJITAMBUSHA CAF

IMEWEKWA FEB. 18,2014 SAA 10:47 JIONI

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi ameondoka leo (Februari 17 mwaka huu) kwenye
Cairo, Misri kujitambulisha kwa uongozi wa juu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF).

Akiwa Cairo, Rais Malinzi ambaye alichaguliwa Oktoba 28 mwaka jana atakutana na Rais wa CAF, Issa Hayatou pamoja na Katibu Mkuu wa shirikisho hilo Hicham El Amrani.

WATATU WAOMBEWA UHAMISHO WA KIMATAIFA
Wachezaji watatu wanaocheza mpira wa miguu nchini Tanzania wameombewa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) ili wakacheze katika nchi za Thailand na Ujerumani.

Mchezaji Khamis Mroki Jamal aliyekuwa na timu ya Daraja la Kwanza ya Polisi Dar es Salaam ameombewa ITC na Chama cha Mpira wa Miguu Thailand (FAT) ili akajiunge na Kabinburi ya nchini humo.

Said Ali Nassor aliyekuwa akichezea FC Turkey ya Zanzibar na Samuel Chuonyo wameombewa na ITC na Chama cha Mpira wa Miguu Ujerumani (DFB) kwa ajili ya kujiunga na klabu ya VfB Eichstatt.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linafanyia kazi maombi hayo na mara taratibu zote zitakapokamilika ikiwemo ridhaa ya klabu zao za hapa Tanzania itatoa ITC hizo.

Post a Comment

0 Comments