Na.Boniface Wambura,IMEWEKWA FEB. 10,2014 SAA 09:46 ALASIRI
Kocha
Msaidizi wa Taifa Stars, Sylvester Marsh ambaye amelazwa Hospitali ya Taifa
Muhimbili (MNH) anasubiri
vipimo vya mwisho ili aweze kuanza matibabu.
Shirikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limemtoa kocha huyo nyumbani kwake jijini
Mwanza na kumleta Dar es Salaam kwa lengo la kuhakikisha anapata matibabu zaidi
na kwa uangalizi wa karibu.
Tayari
majibu ya kipimo cha kwanza yameshapatikana, hivyo yanasubiriwa majibu ya
kipimo kingine ili aweze kuanza rasmi matibabu, lengo likiwa ni kubaini
kitaalamu ugonjwa unaomsumbua.
KIKOSI CHA TWIGA
STARS KUAGWA FEB 12
Timu
ya Twiga Stars itaagwa rasmi Jumatano (Februari 12 mwaka huu) tayari kwa safari
ya Lusaka, Zambia kwa ajili ya mechi ya kwanza ya raundi ya pili ya michuano ya
Afrika kwa Wanawake (AWC) ambayo fainali zake zitafanyika Oktoba mwaka huu
nchini Namibia.
Msafara
wa timu hiyo itakayoondoka kwa ndege ya Fastjet utaongozwa na mjumbe wa Kamati
ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Ahmed Idd Mgoyi.
Hafla
ya kuwaaga wachezaji wa timu hiyo itafanyika saa 5 asubuhi kwenye ofisi za TFF.
Timu hiyo itaondoka Februari 13 mwaka huu alfajiri tayari kwa mechi hiyo
itakayochezeshwa na waamuzi kutoka Rwanda.

0 Comments