Ticker

6/recent/ticker-posts

SOMA TAARIFA KUHUSU KOCHA MSAIDIZI WA TAIFA STARS AMBAYE NI MGONJWA,PAMAOJA NA YA KIKOSI CHA TWIGA STARS AMBACHO KINAAGWA FEB 12

 Na.Boniface Wambura,IMEWEKWA FEB. 10,2014 SAA 09:46 ALASIRI
Kocha Msaidizi wa Taifa Stars, Sylvester Marsh ambaye amelazwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) anasubiri
vipimo vya mwisho ili aweze kuanza matibabu.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limemtoa kocha huyo nyumbani kwake jijini Mwanza na kumleta Dar es Salaam kwa lengo la kuhakikisha anapata matibabu zaidi na kwa uangalizi wa karibu.

Tayari majibu ya kipimo cha kwanza yameshapatikana, hivyo yanasubiriwa majibu ya kipimo kingine ili aweze kuanza rasmi matibabu, lengo likiwa ni kubaini kitaalamu ugonjwa unaomsumbua.

KIKOSI CHA TWIGA STARS KUAGWA FEB 12
Timu ya Twiga Stars itaagwa rasmi Jumatano (Februari 12 mwaka huu) tayari kwa safari ya Lusaka, Zambia kwa ajili ya mechi ya kwanza ya raundi ya pili ya michuano ya Afrika kwa Wanawake (AWC) ambayo fainali zake zitafanyika Oktoba mwaka huu nchini Namibia.

Msafara wa timu hiyo itakayoondoka kwa ndege ya Fastjet utaongozwa na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Ahmed Idd Mgoyi.

Hafla ya kuwaaga wachezaji wa timu hiyo itafanyika saa 5 asubuhi kwenye ofisi za TFF. Timu hiyo itaondoka Februari 13 mwaka huu alfajiri tayari kwa mechi hiyo itakayochezeshwa na waamuzi kutoka Rwanda.


Post a Comment

0 Comments