Mhariri:Herman Kihwili.IMEWEKWA NOVEMBA 11.2013 SAA 03:30 USIKU
Uongozi wa timu ya Azam Fc ya jijini Dar es saalam,umesema
mchakato wa kumpata kocha mpya klabu hiyo bado unaendelea,na
kamati iliyokabiziwa
jukumu la kumtafuta kocha,inaendelea kufanya kazi yake ,ili kuweza kumpata
kocha atakayeweza kulimudu soka la Afrika.
Akizungumza na Jamii na Michezo msemaji wa Azam Fc Jaffari Idd amesema,klabu hiyo inamtafuta
kocha mwenye vigezo,atakayeweza kuichukuwa timu kutoka pale Stewart Hall
alipoacha na kuweza kuwaendeleza,kwa maana bado wanachangamoto nyingi ikiwemo
ligi kuu katika awamu ya pili na mashindano ya kimataifa.
“Ili tuweze kufanya vizuri tunaitaji kupata kocha ambaye
ana uwezo na ambaye anaweza maisha ya Afrika na kujua kwamba wachezaji
wakiafrika wako vipi,kwa mfano unamchukua kocha wakati mwingine kutoka Italy
huko,ujui kitu chochote ambacho kinafanyika hapa Afrika, ajua tabia za wachezaji
wa Afrika.kwahiyo lazima upate kocha ambaye amewai kupata nafasi ya kuweza
kufundisha soka katika nchi yeyote ya kiafrika”alisema Jaffari Idd.
Aidha Jafari iddi ameongeza kuwa kwa sasa zoezi la kumtafuta
kocha ambaye anawafaa bado linashungulikiwa,na endapo litakamilika watatoa
taarifa za kocha yupi ambaye wamempitisha au nani ambaye ametoa maombi ya
kuitaji,ila kwa sasa lazima wapate muda kwa kuwa swala la kumtafuta kocha sio
swala dogo,kwani ukikosea katika swala la kumpata kocha mzuri basi mfumo wote
utakuwa umeharibika.
Pia amekana taarifa zilizoenea jijini kuwa Azam fc inamtaka
kocha wa timu ya Yanga Ernie Brants na
kusema wala hawajapata maombi yeyote kutoka kwa kocha huyo,na wala Azam fc
haijamfuata kocha huyo na kumwambia kama inamuitaji,lakini kama akituma maomgi
ya kutaka kazi ya ukocha katika klabu ya Azam Fc,ataangaliwa sifa zake kama
anafaa au hafai.

0 Comments