Wakala wa Karim Benzema, Djaziri ameliambia gazeti la Kifaransa la Le Journal du Dimanche,kwamba mpango wa benzema kwenda Arsenal haujafanyika.
![]() |
| Majanga kwa Arsene Wenger,Benzema haunzwi,kasema wakala. |
Djaziri
alisema: "uvumi hauwezi kuacha kusikia,Lakini mimi
nawaambia, Karim hawezi kwenda
Arsenal, hakuna hata kidogo mapatano ambayo
yamepatikana, wala mawasiliano.
"Atabaki kukaa Madrid, kuwasili kwa Gareth Bale hakuwezi kutishia Benzema kuondoka. Cristiano Ronaldo na Bale,watacheza nafasi ya ushambuliaji na Karima Benzema atacheza kati."
Benzema ana mkataba na Madrid hadi mwaka 2015 na mazungumzo
yanaendelea juu ya kuongeza mkataba,Karim anaweza kumaliza
kazi yake ndani ya Real,kwani ni klabu ya ndoto yake" alisema wakala huyo Djaziri.
Benzema ambaye ni raia wa Ufaransa alikuwa anahusishwa na uhamisho kwenda Uwanja wa Emirates, na
Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger ana nia ya nguvu ya kuimarisha kikosi chake kwa kiasi
kikubwa, kabla ya tarehe ya mwisho ya usajili ya Septemba 2.

0 Comments