Bingwa wa dunia wa mchezo wa kuruka viunzi,mwana dada Yelena Isinbayeva ameongelea ushoga michezoni, huku kukiwa na maandamano makubwa katika nchi yake ya asili ya Urusi juu ya sheria mpya,ambapo kwa Sasa ni kinyume cha sheria kwa mtu menye umri chini ya miaka 18 kutoa habari kuhusiana na ushoga nchini Urusi.
![]() |
| Mwanadada Yelena Isinbayevana ni bingwa wa dunia wa kuruka viunzi |
Lakini Yelena msimamo wake ni kukosoa wanariadha ambao wanaunga mkono mashoga na wasagaji.
"Tuna hofu sana kuhusu taifa letu kwa sababu wenyewe wanafikiria ni kawaida, " alisema Isinbayeva.
"Kila kitu huja kutokana na historia, Sisi kamwe hatukuwa na matatizo haya katika nchi yetu ya Urusi, na hatutaki kuwa nayo katika siku zijazo,"aliongeza Isinbayeva,baada ya kushinda medali ya tatu ya dunia,siku ya jumanne.
![]() |
| Tunaishi wavulana na wanawake au wanawake na wavulana,na si vinginevyo:Anasema Yelena Isinbayeva |
Msichana huyo bingwa wa michezo ya riadha kutoka urusi,ambaye ana umri wa miaka 31, ana medali mbili za
dhahabu za Olimpiki na anashikilia rekodi ya 28 duniani, pamoja na mafanikio ya ubingwa wa Dunia,amekuwa maarufu na anapendwa sana katika nchi yake.
Kiukweli ameonyesha kitu gani anaamini katika nafasi ya taifa lake juu ya maswala ya ushoga,na kusema kuwa "tunaishi wavulana na wanawake au wanawake na
wavulana,na si vinginevyo.


0 Comments