Ticker

6/recent/ticker-posts

LICHA YA FITINA ZOTE ZA KUWAKOSESHA USINGIZI USIKU KUTWA,FENERBAHCE YACHAPWA BAO 3 KWA BWERERE NA ARSENAL

Licha ya timu ya Arsenal kufanyiwa fitna za kimchezo na mashabiki watukutu na wasiokuwa na adabu  wa timu hiyo ya Fenerbahce  ya uturuki,baada ya kuwapigia kelele kwa kuimba nyimbo zisizokuwa na maana usiku kucha wa kuamkia jana,nje ya hoteli waliofikia timu hiyo ya Arsenal,lakini timu ya Arsenal imeibuka na ushindi mnono wa mabao 3 kwa o dhidi ya majitu hayo ya kituruki usiku wa kuamkia hii leo.
Furaha:Carl Jenkinson, Kieran Gibbs, Theo Walcott, Aaron Ramsey and Olivier Giroud wakisheherekea ushindi
 Magoli yote matatu yalifungwa ndani ya kipindi cha pili, na alikuwa ni Kieran Gibbs ndiye aliyekuwa wa kwanza kabisa kuliona
lango la Fenerbahce katika dakika ya 51,kabla ya Aaron Ramsey kuipatia Arsenal bao la pili bada ya kuachia shuti kali katika dakika ya 64 lililomshinda kipa wa Fenerbahc,na hivyo kuingia moja kwa moja nyavuni,bao la tatu la Arsenal lilifungwa na Olivier Giroud kwa mkwaju wa penalti katika dakika ya 77. 
Hakuna kosa: Olivier Giroud akipiga penalt ya adhabu  baada ya Walcott Theo kufanyiwa makosa  na Mikali Kadlec katika box
Muonekano wa mafaniko:Wenger ameanza vizuri kampeni za ligi ya mabingwa
Refaaa! huonii?
Mchezaji Laurent Koscielny hakumaliza mchezo baada ya kutolewa kutokana na maumivu  baada ya kupasuka karibu na jicho baada ya kupigwa buti  na Pierre Webo. 
Fenarbahce inashiriki katika michuano hii wakati ikisubiri matokeo ya rufaa waliowasilisha kwa shirikisho la soka barani Ulaya baada ya kufungiwa nje ya mashindano haya kwa kosa la kupanga matokeo.
Rufaa hiyo itaamuliwa tarehe 28 siku moja baada ya mchuano wa muaridano na Arsenal ugenini.
Mguu juu: Koscieln,akipigwa boot na Webo katika uso

Koscielny alitolewa na  nafasi yake kuchukuliwa na Carl JENKINSON
kikosi cha Fenerbahce: Demirel 5, Irtegun 4 (Gonul 46, 5), Yobo 6, Bruno Alves 6, Kadlec 5, Topal 5, Meireles 6 (Potuk 82), Emre 6, Sow 4, Webo 4 (Emenike 62, 5), Kuyt . 5  
wachezaji wa akiba wasiotumika: Gunok, KORKMAZ, Baroni, Erkin.
 KADI za njano: Webo, Alves, Kadlec.
Hisia za kuchanganjikiwa: Bacary Sagna na Mertesacker wakipeana tano na kuondoka, lakini Mousa Sow hawezi kuamini  macho yake kilichotokea
kikosi cha Arsenal. Szczesny 7, Sagna 7, Mertesacker 7, Koscielny 6 (JENKINSON 33, 6), Gibbs 7, Rosicky 7, Wilshere 6, Ramsey 8, Cazorla 6, Giroud 6, Walcott 7 (Monreal 87)  
wachezaji wa akiba wasiotumika: Fabianski , Podolski, Sanogo, Frimpong, Gnabry.
KADI za njano: Szczesny.
wafungaji: Gibbs 51, Ramsey 64, Giroud (kalamu) 77.
Mwamuzi: Gianluca Rocchi (Italia)
Walihudhuria: 50,500.

Post a Comment

0 Comments