Chelsea iko katika mazungumzo ya kujaribu bahati yao ya kupata saini ya mchezaji aliye katika malengo ya timu ya Tottenham WILLIAN kutoka Anzhi Makachkala.
![]() |
| Chelsea nayo imetumbukia katika vita vya kutaka saini ya Wilian Anzhi Makachkala. |
klabu hiyo ya darajani imejiingiza katika vita hiyo baada ya
wapinzani wa kutoka London Tottenham kuwa na mazungumzo na WILLIAN mapema jana Alhamisi.
Spurs
walikuwa tayari wameshaweka mzigo wa £ 30m juu ya kiungo huyo,ambaye pia ali ahidiwa mkataba wa miaka mitano kama atatua White Hart Lane.
Lakini mchezaji huyo mwenye umri wa
miaka 25, ambaye pia alikuwa anahusishwa na kijiunga Liverpool mapema
katika majira haya ya joto, inaonekana bado hajatoa msimamo wake na kua muwazi.
![]() |
| Akiwa uwanjani utamtaka! |
Chelsea
tayari wameshasajili katika dirisha hili la usajili,akiwemo mchezaji Andre
Schurrle kutoka Bayer Leverkusen kwa £ 18m,pamoja na Marco van Ginkel kwa £ 8m kutoka Vitesse Arnhem


0 Comments