Mhariri:Herman Kihwili. IMEWEKWA.SEPT.20,2016 SAA 12:11 JIONI
Wabunge
wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania wametangaza mpango wao wa kucheza
mchezo maalum
ambao utasaidia kuchangi fedha kwa ajili ya janga la
tetemeko la Ardhi lililotokea mkoani Kagera juma lililopita.
Mwenyekiti
wa timu ya Bunge William Ngeleja amesema katika kuhakikisha lengo lao
linatimia wameamua kucheza mchezo maaluma mbao utawahusisha wabunge
wanaozishangilia klabu kongwe hapa nchini za Simba na Yanga ili kuleta
chachu ya ushindani.
Amesema
dhumuni lao linapaswa kuungwa mkono na watanzania kwa kwenda uwanjani
kushuhudia mchezo huo maalum, ambao kwa upande mwingine utatoa burudani.
![]() |
| Single Mtambalike (Rich Rich) akizungumza |
Kwa
upande wa muwakilishi wa timu ya wasanii wa filamu (Bongo Movie) Single
Mtambalike (Rich Rich) ametoa wito kwa watanzania bila kujali itikadi
za kimichezo kufika uwanjani siku ya jumapili kwa lengo la kushuhudia
burudani pamoja na kuchangia sehemu ya fedha zitakazowasaidia waathirika
wa janga la tetemeko la ardhi.
Pia
mewataka wasanii wenzake kutumia majukwaa ya mitandao ya kijamii ili
kuwavuta watu wengine wa ndani nan je ya nchi ili waweze kufika uwanjani
siku hiyo, kwa lengo la kuonyesha umoja na mshikamano kwa kuwasaidia
watanzania waliofikwa na matatizo.
Naye
kocha mchezaji wa timu ya wasanii wa muziki (Bongo Fleva) Karama Masoud
(Kalapina) ametamba kuwa na kikosi kizuri na ametoa tahadhari kwa
wapinzani wao Bongo Movie kutarajia kadhia kubwa ya kupoteza mchezo huo
muhimua mbao utaingia katika historia ya nchi ya Tanzania.
ANGALIA PICHA







0 Comments