Mhariri:Herman Kihwili. IMEWEKWA.Jun 14,2016 SAA 02:01 USIKU
Timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 (Serengeti Boys), hii leo kimeanza mazoezi rasmi ya kujiandaa na mchezo wa
kuwani nafasi ya kufuzu kwa fainali za mataifa ya Afrika kwa vijana dhidi ya Shelisheli ambao umepangwa kuchezwa mwishoni mwa mwezi huu jijini Dar es salaam.
Timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 (Serengeti Boys), hii leo kimeanza mazoezi rasmi ya kujiandaa na mchezo wa
kuwani nafasi ya kufuzu kwa fainali za mataifa ya Afrika kwa vijana dhidi ya Shelisheli ambao umepangwa kuchezwa mwishoni mwa mwezi huu jijini Dar es salaam.
Kocha mkuu wa Serengeti Boys, Bakari Shime amesema vijana wote wapo katika hali nzuri na utaratibu wa mazoezi waliouandaa utakua unachukua nafasi yake asubihi na jioni katika uwanja wa Karume jijini Dar es salaam.
SIKILIZA HAPA
HHata hivyo Shime ameendelea kuwaomba mashabiki wa soka nchini kuwa snjari ya kikosi chake ambacho kwa sasa ndicho kilichosalia katika majukumu ya kuitafutia nafasi Tanzania ya kucheza katika fainali kubwa za barani Afrika.
Shime ameongeza kwamba katika mchakato wa maandalizi ya kikosi hicho cha timu ya vijana chini ya umri wa miaka 17, hakutakua na mchezo wowote za kimataifa wa kirafiki zaidi ya kutumia mafunzo waliyoyapata kwenye michezo kadhaa waliyowahi kucheza ikiwepo ile waliyokwenda nchini India.
KWA TAARIFA,BREAKING NEWS,RATIBA PAMOJA NA MATOKEO YA MECHI MBALIMBALI,LIKE PAGE YA FACEBOOK BONYEZA HAPA (Jamii na Michezo) .
0 Comments