Ticker

6/recent/ticker-posts

AUDIO:CHAMA CHA SOKA TEMEKE CHATANGAZA UCHAGUZI NA OFISA HABARI BEN MWANANTALA

Mhariri:Herman Kihwili. IMEWEKWA.JULY.05,2015 SAA 10:35 JIONI
Ofisa habari wa chama cha mpira wa miguu wilaya ya Temeke (katikati)Ben Mwanantala akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani ) kulia ni katibu mkuu wa chama hiko Hassan Mustapha

Chama cha mpira wa miguu wilaya ya Temeke (TEFA) hii leo Kimetangaza kuanza rasmi mchaakato wa uchaguzi wa chama hiko
utakaofanyika tarehe 16 mwezi wa nane mwaka huu.
kikao cha kamati ya utendaji kikiendelea
Akizungumza na waandishi wa habari hii leo katibu mkuu wa chama hiko Hassan Mustapha amesema,mara baada ya kufanyika kwa kikao cha kamati ya utendaji,wameamua zoezi rasmi la kuchukua na kurudisha fomu za kuomba uongozi katika chama hiko,litakuwa rasmi tarehe 7 mwezi wa 7 mwaka huu.

Katika hatua nyingine  Hassan Mustapha amemtangaza Ofisa Habari wa chama cha mpira wa miguu wilaya ya Temeke (TEFA) ambaye ni Ben Mwanantala.

Akizungumza mara baada ya kutangazwa kama ofisa habari wa chama cha mpira wa miguu wilaya ya Temeke (TEFA)Ben Mwana ntala amekishukuru chama hiko kwa kumuamini na kumpa nafasi hiyo.


MSIKILIZE KATIBU WA TEFA HASSAN MUSTAFA NA BEN MWANANTALA


RATIBA YA MATUKIO YA UCHAGUZI WA CHAMA CHA MPIRA WA MIGUU WILAYA YA TEMEKE 


KWA TAARIFA,BREAKING NEWS,RATIBA PAMOJA NA MATOKEO YA MECHI MBALIMBALI,LIKE PAGE YA FACEBOOK  BONYEZA HAPA (Jamii na Michezo)

Post a Comment

0 Comments