Ticker

6/recent/ticker-posts

DAVID LUIZ ANAKUTANA NA TIMU YAKE YA ZAMANI LEO,HIKI NDICHO ALICHOKISEMA

Mhariri:Herman Kihwili IMEWEKWA.Feb.17,2015 SAA 08:34 USIKU
Beki wa Paris Saint-Germain David Luiz anasema anatarajia upinzani mgumu wakati timu yake hiyo itakapokutana na
klabu yake ya zamani ya Chelsea katika Ligi ya Mabingwa siku ya leo Jumanne.

Luiz aliondoka Stamford Bridge na kutua Parc de Princes kwa ada ya uhamisho £ 50 msimu uliopita na mchezaji huyo anasema anaamini kuwa Chelsea imewekeza fedha vizuri.

Ada iliyopokelewa kwa ajili Luiz ilimsaidia bosi wa Chelsea Jose Mourinho kumleta Diego Costa, Cesc Fabregas na Filipe Luis  nyota wa kimataifa wa Brazil,na Luiz anaamini kikosi cha Mourinho  kina nguvu kwa sababu ya wachezaji walioongezeka.

David Luiz  anasema kuwa anaamini pia PSG itakuwa klabu bingwa miaka si mingi,kwani kila siku klabu hiyo imekuwa na maendeleo.


"Katika mchezo, hakutakuwa na pengo. Kuna timu mbili  nzuri, wachezaji bora na makocha wawili wanye vipaji. Tunahitaji kuthibitisha jinsi tutakapofika uwanjani."
"Wao wana wachezaji wawili au watatu waliojiunga na wenye viwango vya juu, kama Fabregas na Diego. Wana nguvu mwaka huu," alisema.



Timu hizo mbili zilikukutana katika robo fainali ya mashindano ya msimu uliopita, na Chelsea kufaidika na bao la ugenini baada ya kumalizika mchezo kwa jumla ya sare ya mabao 3-3 .
Luiz alifunga bao mwenyewe katika mchezo wa kwanza wa chelsea iliomalizika kwa Chelsea kufungwa 3-1 na Paris, kabla ya kushinda katika mechi ya pili 2-0.
"Mwaka jana mimi nilifunga bao Langu ya kwanza kwa PSG," aliongeza. "Kama mimi nita funga dhidi ya Chelsea sitashangilia kwa heshima, lakini nitakuwa na furaha.Nataka kufudhu, kama nilivyofudhu mwaka jana, lakini nataka kufudhu na PSG. "
Lakini katika hatua nyingine Meneja wa PSG, Laurent Blanc pia anatarajia mambo mazuri  na aliwaonya wachezaji wake kutoshindwa kukabiliana na Mourinho mwenye akili katika michezo.


KWA TAARIFA,BREAKING NEWS,RATIBA PAMOJA NA MATOKEO YA MECHI MBALIMBALI,LIKE PAGE YA FACEBOOK  BONYEZA HAPA (Jamii na Michezo) . 

Post a Comment

0 Comments