Ticker

6/recent/ticker-posts

MICHUANO YA LIGI YA MKOA DAR INAENDELEA.

Mhariri:Herman Kihwili IMEWEKWA.Feb.16,2015 SAA 08:46 MCHANA
Wachezaji wa Ugimbi United kulia ni Abdala Kisanda Paulo Semkiwa
Michuano ya ligi ya mkoa wa Dar es salaam inaendelea tena wiki hii kwa timu 8 kushuka katika viwanja tofauti,kupambana
ili kuusaka ubingwa huo pamoja na kupata nafasi ya kuingia katika ligi daraja la pili taifa.

Mechi za leo Februari 16,2015/Azania Ngano watakipiga dhidi ya Yanga U20 (Katika uwanja wa Karume),Stakishari watacheza na FFU (uwanja wa B.Mkapa),Changanyikeni wataumana dhidi ya Tuamoyo (uwanja wa MWL/Nyerere) na New Kunduchi wataoneshana kazi dhidi ya Sinza Stars (uwanja wa Kines).

Kivumbi hicho kitaendelea tena kesho Kutwa Februari 18,2015 kwa Simba U20 kucheza na Ukonga UTD (Uwanja wa karume),Red Coast watacheza dhidi ya Shababi (MWL/Nyerere),Zakhem watacheza na Sifa UTD ( Uwanja wa Bandari) na Beirahotspurs watakipiga dhidi ya Pan African (uwanja wa Kines).

KWA TAARIFA,BREAKING NEWS,RATIBA PAMOJA NA MATOKEO YA MECHI MBALIMBALI,LIKE PAGE YA FACEBOOK  BONYEZA HAPA (Jamii na Michezo) . 

Post a Comment

0 Comments