Mhariri:Herman kihwili,IMEWEKWA.APR. 29,2014 SAA 03:23 ASUBUHI
Gary
Neville angependa kuona Manchester United inaendeleza tamaduni yao kwa
kumteua mameneja kutoka Uingereza - na
anataka Ryan Giggs kupewa nafasi hiyo.
Kocha
wa Uholanzi Louis van Gaal amekuwa akipendekezwa kuchukuwa kazi hiyo na klabu
alithibitisha siku ya Jumatatu kuwa wao walifanya mazungumzo pamoja naye,
lakini bado wataendelea kuweka wazi watu waliopendekezwa.
Hata
hivyo, Neville anasema kwamba kumchagua kocha huyo mwenye umri wa miaka 62 ambaye
hajawahi kufanya kazi katika Premier League ni hatari kwa
kuungwa mkono,tofauti na mchezaji mwenzake wa zamani Giggs ambaye ameanza kushawishi baada ya
kuongozwa timu kwa kushinda 4-0 dhidi ya Norwich siku ya Jumamosi
"Yeye ni mzoefu, alishinda vikombe katika nchi mbalimbali na amefundisha klabu kubwa Ulaya.," Alisema alipokuwa akiongea na Monday Night Football.
"Anapendekezwa kwa wakati huu na tunajua siku hizi uzito wa
uvumi katika vyombo vya habari , wakati ambapo ajira inakuwepo.
Nadhani wakati unawafanya kuelekeza kwake".
"Ningependa kumuonekana Ryan katika michezo miwili au mitatu. Alianza vizuri siku ya Jumamosi, hivyo basi kuwa na michezo miwili au mitatu zaidi ili kumuona kama atafaa katika nafasi na kama anaweza kukalia kiti basi apewe jukumu hilo".
"Sifikirii hili kwa vyovyote vile, kwamba Kuna wazo kuwa Ryan hana uzoefu
lakini yeye anaijua klabu na kuna wazo kwamba Van Gaal ana uzoefu
mkubwa,sawa, lakini hajui Premier League".
"Mwishoni
mwa siku wamiliki watafanya kile wanachotaka kufanya.watampendekeza kwa vyovyote vile mwenye uzoefu , lakini mimi binafsi ningependa kuona
meneja aliyefanya kazi Uingereza anateuliwa kwa sababu Manchester United daima ni maalumu
kwa mameneja wa Uingereza".
" itabidi tusubiri na kuona." alisema Gary
Neville
0 Comments