IMEWEKWA March. 07,2014 SAA 03:03 USIKU
Ligi
Kuu ya Vodacom (VPL) inaendelea kesho (Machi 8 mwaka huu) kwa mechi tatu ambapo
Coastal Union
itaumana na Ashanti United kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini
Tanga.
Ruvu
Shooting itaikaribisha Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Mabatini, Mlandizi mkoani
Pwania wakati Mbeya City itacheza na Rhino Rangers kwenye Uwanja wa Kumbukumbu
ya Sokoine jijini Mbeya.
Mechi
za Jumapili (Machi 9 mwaka huu) ni Tanzania Prisons na Simba kwenye Uwanja wa
Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya, na JKT Ruvu na Mtibwa Sugar zitacheza
Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi, Dar es Salaam.
FDL
KUTIMUA VUMBI WIKIENDI
Ligi Daraja la Kwanza (FDL) inaendelea
wikiendi hii kwa timu za makundi yote matatu kushuka kwenye viwanja tofauti
nchini ambapo kesho (Machi 8 mwaka huu) Tessema itacheza na Transit Camp kwenye
Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.
Kundi B ni Burkina Faso vs Kurugenzi
(Jamhuri, Morogoro) wakati C Polisi Tabora vs Mwadui (Ali Hassan Mwinyi), Stand
United vs Pamba (Kambarage), Polisi Mara vs Kanembwa JKT (Karume) na Polisi
Dodoma vs Toto Africans (Jamhuri, Morogoro).
Mechi za Jumapili ni kundi A, African
Lyon vs Polisi Dar (Karume), Villa Squad vs Friends Rangers (Mabatini, Pwani)
na Ndanda vs Green Warriors (Nangwanda Sijaona, Mtwara). Kundi B ni Polisi
Morogoro vs Majimaji (Jamhuri, Morogoro) na Mlale JKT vs Lipuli (Majimaji,
Songea).

0 Comments