Ticker

6/recent/ticker-posts

UGANDA KUJIPANGA NA ZAMBIA KWA AJILI YA MECHI ZA KIRAFIKI

 Mhariri:Herman Kihwili,IMEWEKWA FEB. 20,2014 SAA 01:20 USIKU 
Uganda Cranes itakutana timu ya Zambia Chipolopolo mwezi ujao kwa ajili ya mechi mbili za kirafiki za kujiandaa na kufuzu kwa 
Kombe la Mataifa ya Afrika 2015.

Shirikisho la Vyama vya  soka Uganda (Fufa) limethibitisha leo Alhamisi kwamba wao wamekubaliana na wenzao wa Chama cha Soka cha Zambia (FAZ), kwa kila mmoja kufanya majaribio kabla ya kampeni hiyo.

Timu hizo mbili zitakutana Machi 5 katika  uwanja waNdola uliopo Zambia,kama mchezo wa Uganda wa kujiandaa kwa ajili ya mzunguko wote wa awali wa kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON)  mwaka 2015 na Zambia kuendelea kujiweka vizuri kutokana na hatua ya makundi mwezi septemba.

Post a Comment

0 Comments