Ticker

6/recent/ticker-posts

HIKI NDICHO JOSE MOURINHO ANACHOTAKA KUKIFANYA KWA KUMCHUKUA MCHEZAJI HUYU MWENYE MIAKA 40

 Mhariri:Herman Kihwili,IMEWEKWA FEB. 21,2014 SAA 10:10 USIKU 

Kocha wa Chelsea Jose Mourinho ameunda hoja ya kumchukuwa mchezaji wa  Inter's Javier Zanetti kwenda katika klabu hiyo ya Stamford Bridge na kuwa kama mchezaji mwenye jukumu la
ukocha,imefahamika hivi karibuni.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 40 , ambaye alihamia San Siro mwaka 1995, alifanya kazi chini ya Mourinho kwa miaka miwili katika klabu ya Internazionale.

Zanetti, ingawa mkataba wake na klabu yake unamalizika mwezi Juni , lakini familia yake ina makazi katika mji wa  Milan, haija fahamika kama atazingatia pendekezo kama angeweza kuungano na Mourinho.

Kocha huyo  mwenye umri wa miaka 51 , amependekeza kwamba MuArgentina huyo kujiunga na wafanyakazi wa safu ya ndani kwa mwaka 2014-15 kabla ya kampeni  ya kuchukua nafasi ndani ya vyumba vya ndani vya timu kwa msimu unaofuata.  

Mourinho ana nia ya kuongeza uzoefu na kushinda mataji makubwa, na mipango yake imekuwa ikipitishwa na mmiliki Roman Abramovich.

Zanetti, hata hivyo, bado ana nia ya kusalia Inter kwa  mazungumzo na rais Erick Thohir kufafanua msimamo wake katika klabu na kama angekuwa na uwezo wa kuanza kazi yake ya kufundisha akiwa Italia.  

Mchezaji huyo wa kimataifa wa zamani wa Argentina , ambaye ana vikombe 145  kwa nchi yake, anaona Milan kama ndio nyumbani kwake na itachukua muda kwa Mourinho kumrubuni kwa malipo na kuhamisha makazi yake yawe magharibi ya London.



USISAHAU KULIKE PAGE YA FACEBOOK,TAFUTA  Jamii na Michezo

Post a Comment

0 Comments