Mhariri:Herman Kihwili,IMEWEKWA FEB. 19,2014 SAA 11:19 JIONI
Manuel
Pellegrini anaamini mwamuzi Jonas Eriksson aliyeamua mchezo wa
Manchester City ambao walifungwa mabao 2-0 na
Barcelona katika Ligi ya
Mabingwa Ulaya,usiku wa kuamia hii leo,aliipendelea Barca mwanzo mpaka mwisho wa mchezo huo
City imefungwa katika mechi ya kwanza hatua ya 16 Bora,ambapo walikuwa na matumaini ya kushinda,lakini sasa wana mlima wa kupanda dhini ya Wacatalunya hao.
Bosi huyo wa
City, ambaye alimuona Dani Alves akipachika bao la pili kwa Barca katika hatua za
mwisho, aliiambia Sky Sports: "Bila shaka mimi nina malalamiko, si tu kwa
ajili ya adhabu na kadi nyekundu".
"Nadhani katika mechi nzima hatukuwa na mwamuzi mwenye uadilifu kwa timu zote mbili."
"Yeye
aliamua mchezo. Aliamua mchezo kwa sababu kulikuwa na faulo ya (Sergio)
Busquets dhidi ya Navas. Mwamuzi aliona makosa zaidi ya matatu,lakini hakupiga
filimbi na baada ya faulo kutoka kwa Demichelis moja kwa moja akamtoa nje kwa kadi nyekundu,ilikuwa
si adhabu"
"Makosa muhimu dhidi ya timu kubwa kufanya kama Barcelona ni vigumu kushinda."
City sasa wanahitaji kushinda angalau mara mbili katika mchezo utakaopingwa katika uwanja wa Nou Camp March 12.
0 Comments