Ticker

6/recent/ticker-posts

WENGER ATOA YA MOYONI,SEMA HANA AMANI AKIMUONA ROBIN VAN PERSIE AKIWA NA JEZI YA MANCHESTER UNITED

Mhariri:Herman Kihwili.IMEWEKWA NOVEMBA 8.2013 SAA 08:21 USIKU

Arsene Wenger amekubali kuwa anajisikia tofauti(vigumu) kwa yeye kumuona Robin van Persie akiwa amevaa shati nyingine
yoyote zaidi ya Arsenal.
 Wenger atakutana na MDutchman huyo kwa mara nyingine tena siku ya Jumapili,ambapo timu hiyo inayoongoza Ligi Kuu itakutana na Manchester United katika uwanja wa Old Trafford.
Ingawa ni zaidi ya mwaka mmoja tangu kumuuzwa Van Persie kwa Sir Alex Ferguson kwa 24million £, Wenger anasema hawezi kukaa vizuri akimuona mshambuliaji huyo katika kikosi cha United. 
Msimu wa kwanza wa Van Persie uliomalizika ndani ya Old Trafford,aliweza kuipatia ubingwa wa kwanza wa Ligi Kuu', miaka nane baada ya Wenger kumpeleka England kutoka Feyenoord. 
"Bila shaka ni ajabu kwa sababu kwangu mimi, yeye ni mtu wa Arsenal," Wenger alisema. 
"Mimi nilimchukua yeye wakati alikuwa mchezaji kijana sana,tulikuwa pamoja katika njia ya vipindi vigumu sana. Na akawa mchezaji wa daraja la dunia, kwangu mimi yeye ni mchezaji wa Arsenal." 
Wenger pia umebaini kuwa ni kocha wa zamani msaidizi wa United Rene Meulensteen,ndiye aliyeshawishi  van Persie kujiunga na kikosi hiko cha united. 
"Robin van Persie alikuwa ameshawishika na kocha wa Kiholanzi ambaye alikuwa katika klabu ya Manchester United sasa anafundisha Anzhi Makhachkala, (hivyo) kwamba alicheza sehemu kubwa ya uhamisho wa mchezaji huyu," Wenger alisema. 

Post a Comment

0 Comments