Ticker

6/recent/ticker-posts

WALCOTT KUKOSA MECHI ZA KUFUZU KOMBE LA DUNIA NA TIMU YAKE YA ENGLAND

  Mhariri:Herman Kihwili,IMEWEKWA SEPT 24,2013 SAA 3:35 USIKU
Winga  wa klabu ya Arsenal Theo Walcott atakuwa nje katika mechi mbili za timu yake ya taifa la England katika mechi za kufuzu Kombe la Dunia  kwa sababu anahitaji matibabu kwa ajili ya
maumivu ya tumbo,hayo yamesemwa na uongozi wa klabu yake hiyo inayoshiriki ligi kuu.
"Atakuwa anatibiwa nchini Ujerumani siku ya  Jumatano na, kwa sababu hiyo, tunaweza kuanza Rehab kwa ajili yake mara moja," Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger aliiambia tovuti ya klabu (www.arsenalcom)
 "Sisi tunamatumaini ya kushughulikia swala hili  kwa haraka na yeye lazima atakosa  mechi nyingi za  Arsenal  Lakini pia atakosa michi zijazo za kimataifa na Uingereza."
Uingereza,wako juu ya pointi  moja kwa timu ya Ukraine na Montenegro katika kundi H, ni kutokana na kucheza na timu ya Montenegro na Poland wakiwa  nyumbani Oktoba 11 na 15 katika michezo yao ya mwisho ya kufuzu  kwa ajili ya mashindano ya mwaka ujao nchini Brazil.
Walcott amekosa ushindi wa Arsenal dhidi ya  Stoke City Jumapili,ushindi uliowaweka juu  Gunners katika  Ligi Kuu baada ya mchezaji huyo kupata matitizo hayo ya ukuta wake wa nyuma  ya tumbo.
 "Siyo ngiri, lakini inafanana kidogo kimuundo na  tatizo hilo katika tumbo lake," alisema Wenger.

Post a Comment

0 Comments