Ticker

6/recent/ticker-posts

RHINO KUIKARIBISHA ASHANTI ALI HASSAN MWINYI

 Na.Boniface Wambura,.IMEWEKWA SEPT. 24,2013 SAA 11:00JIONI
Rhino Rangers na Ashanti United zinapambana katika mechi pekee ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) itakayochezwa kesho
(Septemba 25 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora.
Wakati Rhino Rangers ilitoka sare ya bao 1-1 katika mechi yake iliyopita jijini Tanga dhidi ya Mgambo Shooting Stars, Ashanti United inashuka uwanjani huku ikiwa na kumbukumbu mbaya ya kutandikwa mabao 3-0 na Kagera Sugar katika mechi iliyochezwa Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.

TWIGA STARS YAPANGIWA ZAMBIA AWC
Timu ya Taifa ya mpira wa miguu ya wanawake (Twiga Stars) imepangiwa kucheza na Zambia katika mechi za kutafuta tiketi ya kucheza Fainali za Afrika kwa Wanawake (AWC) zitakazofanyika mwakani nchini Namibia.

Twiga Stars itaanzia ugenini jijini Lusaka ambapo mechi ya kwanza itachezwa kati ya Februari 13 na 15 mwakani wakati ile ya marudiano itafanyika kati ya Februari 28 na Machi 2 mwakani jijini Dar es Salaam.

Iwapo Twiga Stars itafanikiwa kuitoa Zambia, raundi ya pili ambayo ndiyo ya mwisho itacheza na mshindi kati ya Botswana na Zimbabwe. Mechi ya kwanza itakuwa Dar es Salaam kati ya Mei 23 na 25 mwakani wakati ile ya marudiano itakuwa kati ya Juni 6 na 8 mwakani.

Nchi 25 zimeingia katika mashindano huku mabingwa watetezi Equatorial Guinea, makamu bingwa Afrika Kusini na Cameroon iliyoshika nafasi ya tatu katika fainali zilizopita zikiingia moja kwa moja katika raundi ya pili.


Post a Comment

0 Comments