Ticker

6/recent/ticker-posts

BEI YA MAJI ITAPANDA IWAPO WANANCHI NA MAMLAKA WATAKUBALIANA:SAID MECK SADIKI

Na.Herman Kihwili.IMEWEKWA SEPT. 25,2013 SAA 3:31USIKU
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Said Meck Sadiki akizungumza hii leo
Mamlaka ya Majisafi na majitaka Jijini Dar es Salaam,-DAWASA, leo imetoa mapendekezo kuhusiana na maombi ya kurekebisha bei za maji. 
Akizungumza katika mkutano wa DAWASA, Mgeni rasmi ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki amesema
kuwa, bei ya maji itapanda iwapo tu wananchi na mamlaka husika watakubaliana katika mkutano huo.
Lakini pia Said Meck Sadiki alilalamika kwamba  mkutano hakukuwa na wanachi wengi waliohudhulia katika mkutano huo,(lakili bei ikipanda wao ndio wakwanza kulalamika)
Aidha Sadiki ameongeza kuwa, Serikali imekuwa ikipata lawama kutokaa na baadhi ya watu kuharibu miundo mbinu ya maji na amewataka watu hao kuacha kufanya hivyo kwani sheria itafuata mkondo wake.
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Said Meck Sadiki akiondoka baada ya kuhutumia katika mkutano huo
 DAWASA imeamua kuandaa mkutano huo ili kupata maoni ya wananchi kwani kwa sasa inakabiliwa na changamoto ya mapato ya kuweza kumudu gharama za uzalishaji na usambazaji.
DAWASA ambayo ilianzaisha Tarehe 4/4/ 1997 na baada ya kuunganishwa NUWA na DSSA,lakini sheria ililekebishwa mwaka 1999 kuruhusu ubinafsishaji washunguli za DAWASA,na mikoa inayohudumiwa na DAWASA ni pamoja na Bagamoyo,Kibaha na Dar es saalam.

Post a Comment

0 Comments