IMEWEKWA SEPT 25,2013 SAA 1:25 USIKU
Mashindano ya mpira wa magongo kwa mataifa ya Afrika
yaliyopangiwa kuanza Alhamisi wiki hii na kusogezwa mbele hadi tarehe 1 Octoba mjini Nairobi huenda
yakaahirishwa kutokana na
mkasa wa jumba la Westgate lililovamiwa na
magaida wa Al Shabaab, na zaidi ya watu sitini kuuawa.![]() |
| Mwana mama aliyejeruhiwa akitolewa nje ya jengo hilo ili kufanyiwa matibabu,na kwa nyuma anaonekana mtu ambaye amepoteza maisha kutokana na kupigwa risasi |
Mwenyekiti wa chama cha mchezo wa magongo cha
Kenya Nashon Randiak anasema shirikisho la kimataifa,FIH, lina wasiwasi
kuhusu usalama wa wachezaji mjini Nairobi baada ya magaidi wa Al Shabaab
kulivamia jengo la kibiashara la Westgate jijini Nairobi.
![]() |
| Hali ilinyokuwa katika jengo la kibiashara la Westgate jijini Nairobi baada ya uvamizi wa magaida wa Al Shabaab |
Licha ya Randiak kuwaeleza kwamba
hali sasa ni shwari baada ya magaidi wote kuuwa na wanajeshi wa Kenya
shirikisho la kimataifa limesema linataka mkuu wa polisi nchini Kenya
kuwahakikisha usalama wa wachezaji.
Randiak ameshangazwa na msimamo huo akisema
mashambulizi ya magaidi hutokea kote duniani hivyo anashangaa ni kwanini
hili la Kenya linachukuliwa ni kama la kipekee..
Mataifa yanayotarajiwa kushiriki kwa wanaume ni
Kenya, Ghana na Afrika Kusini na kwa wanawake ni Kenya, Tanzania,Ghana
na Afrika Kusini. Timu ya Tanzania ikiongozwa na katibu wa chama cha
magongo mkoa wa Dar es salaam Mnonda Magani tayari imeshawasili mjini
Nairobi.
![]() |
| katibu mkuu wa chama cha mpira wa magongo mkoa wa Dar es salaam(DRHA) Mnonda Magani |
Timu ambazo zimejiondoa kwa sababu mbali mbali na sio hiyo ya Westgate ni pamoja na Nigeria, Namibia, Misri na Ushelisheli.
WACHEZAJI WA TANZANIA WALIOKWENDA KENYA
Nahodha
ni Magreth Eliud,na wachezaji wengine ni Audia Mkucha,Kidawa
Selemani,Eva Elias,Miriam Ngomaitara,Mary Muhina,Salome Thomas,Joyce
Esabius,Hadija Mohamed,Frola Simbamkole,Mariam Zawad,Leah Shani,Winfida
Gowele,Hawa Musa,Happy Ngoko na Sophia Kumpaha.
CHANZO:BBC swahili na jamiinamichezo.blogspot.com




0 Comments