Ticker

6/recent/ticker-posts

ROBERT LEWANDOWSKI ATHIBITISHA KUJIUNGA NA BAYERN IFIKAPO JANUARI

Mhariri:Herman Kihwili,IMEWEKWA SEPT 26,2013 SAA 9:25 USIKU
Robert Lewandoski amethibitisha  kuondoka Dortmund ifikapo Januari
Mshambuliaji wa Borussia Dortmund Robert Lewandowski ameviambia  vyombo vya habari vya Ujerumani kwamba anatarajia
kuthibitisha kujiunga na  Bayern Munich mnamo mwezi Januari.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25  kwa muda mrefu amekuwa akihusishwa na vyombo vya habari  zaidi  duniani kutaka kujiunga na Bayern.
Taarifa zinasema atapewa mkataba wa miaka minne na Bayern - kuanza kwa msimu ujao.Alipoulizwa kama angeweza kuthibitisha hoja ya kujiunga na Bayern mwezi Januari, Lewandowski aliiambia Sport 1: "Ndiyo, kwa sababu siwezi kusaini mkataba mpya mwezi Januari."
Lakini pia Lewandowski alikaliliwa  akiiambia  Sky Deutschland kwamba  anaamini kuwa anaweza hata kuondoka kabla ya majira ya joto. 
Kwa sasa, siwezi kusema lolote," aliongeza mchezaji huyo wa  kimataifa wa Poland. "Kwa kawaida, naweza tu kutangaza rasmi mwezi Januari. 
"Wakati huu, bado ni mapema mno na itabidi kusubiri kidogo Lakini. Nadhani,naweza kuondoka ikifika Januari." 

Post a Comment

0 Comments