Na.Boniface Wambura pamoja na Herman kihihwili,IMEWEKWA AGOSTI 27,2013 SAA 10:40 jioni
Ligi
Kuu ya Vodacom (VPL) inaingia raundi ya pili kesho (Agosti 24 mwaka
huu) kwa timu zote 14 kuwa viwanjani huku macho na masikio ya washabiki
wengi yakielekezwa kwenye mechi kati ya Yanga na Coastal Union.
Mechi
hiyo itachezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10.30 jioni
kwa kiingilio cha sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000.
Mwamuzi Martin Saanya wa Morogoro ndiye atakayepuliza filimbi wakati
Kamishna atakuwa Omari Walii kutoka Arusha.
Kamishna atakuwa Omari Walii kutoka Arusha.
Mtibwa
Sugar itaikaribisha Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Manungu ulioko
Turiani mkoani Morogoro wakati Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora
utakuwa mwenyeji wa pambano kati ya wenyeji Rhino Rangers na Azam.
Vumbi
lingine litatimka kwenye Uwanja wa Mabatini ulioko Mlandizi mkoani
Pwani wakati maafande wa JKT Ruvu watakapokwaruzana na wenzao wa
Tanzania Prisons kutoka Mbeya. Mbeya City na Ruvu Shooting zitacheza
kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.
Jiji
la Tanga litakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Mgambo Shooting na Ashanti
United itakayochezwa kwenye Uwanja wa Mkwakwani. Oljoro JKT itakuwa
mwenyeji wa Simba kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Kaluta Amri
Abeid jijini Arusha.

0 Comments