Klabu ya Real Madrid imetoa ofa mbili tofauti kawa ajili ya kumchukua winga Gareth Bale na kusuburi kuona klabu ya Tottenham Hotspur inachagua ofa moja.
![]() |
Gareth Bale:Anataka kufanywa kuwa mchezaji mwenye thamani sana duniani |
Imetoa ofa ya kwanza ambayo ni ya €100m (£ 86m) malipo yatayo ambatana na mkataba wa miaka mitatu hadi minne,ambayo itakuwa imeishinda ofa iliyovuka rekodi ya dunia kutoka Manchesta united kwa Cristian Ronaldo ya £80m.
Nyingine ni malipo ambayo itakuwa karibu na £ 70m,ofa hii itakuwa inamfanya kuwa mchezaji wa ghali sana,kwani itamuwezesha kumfanya mchezaji anayelipwa mshahala mkubwa na wenye thamania kuliko Cristian Ronaldo.
Lakini Katika hatua nyingine kocha wa Barcelona Gerardo Martino imelaani kitendo cha Real Madrid kutaka kumsainisha Gareth Bale kwa ofa hiyo ambayo itavunja rekori ya dunia na kusema uhamisho huo ni ukosefu wa heshima.
Martino amesema: 'Bale ni mchezaji mzuri lakini idadi hiyo ya euros 100m ni kama kuwa na ukosefu wa heshima kwa ajili ya mchezo wa soka dunia.
![]() |
Amechukizwa:Gerardo Martino anasema Bale ni mchezaji mzuri lakini idadi hiyo ya euros 100m ni kama kuwa na ukosefu wa heshima kwa ajili ya mchezo wa soka dunia.
|
Wakati huo huo Kocha wa Spurs Andre Villas-Boaz hatarajii Bale kuwepo White Hart Lane siku ya kesho katika mchezo dhidi ya Swansea,kwa sababu anaweza kugeuka kwa sababu ya mpango wake wa kuamia Real Madrid.
![]() |
Anawasiwasi: bosi wa Spurs Andre Villas-Boaz hafikirii Bale atakuwepo kwa katka mchezo dhidi ya Swansea
|



0 Comments