Na john Piter. IMEWEKWA AGOSTI 18,2013 SAA 8:30 MCHANA
Chama cha mpira wa
miguu kwa mkoa wa Dar es saalam (DRFA) leo kimeendesha semina ya siku moja kwa
klabu 11 za Mkoa wa Dar es Salaa zinazoshiriki Ligi Kuu ya na Ligi Daraja la
Kwanza Tanzania Bara ili kuboresha weledi na hatimaye kufanya vizuri.
![]() |
| Mbunge wa Ilala, Mussa Hassan Zungu:alifungua semina badala ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadik,kama ilivyotangazwa |
Akifungua semina
hiyo Mh.Mussa hassan Zungu ambaye ni mbunge wa Ilala,amesema ili kuwa kocha
bora lazima ujue sheria zote za
mchezo wa soka ili ulete mafanikio ya soka,
mchezo wa soka ili ulete mafanikio ya soka,
Lakini pia
zunguwakati wa hutuba yake, aligusia swala la ushirikina katika soka,na kusema,
uchawi katika soka hakuna kama hufanyi mazoezi ya kutosha,kamwe hauwezi kufanya
chochote katika soka.
MOJA YA JAMBO LA
KUFURAHISHA NI PALE ILIPOTOLEWA HISTORIA YA MATUMIZI YA KADI NYEKUNDU NA
NJANO KUTUMIKA KATIKA MCHEZO WA SOKA.
Miaka ya nyuma
katika kombe la dunia,kulikuwa na mechi kati ya Colombia na Argentina,refa
alikuwa muingereza, baada ya kutoelewana kwa Lugha kati ya wachezaji na refa
juu ya makosa ambayo yalitolewa pale uwanjani,mpira ulisimama kwa dakika kadhaa.Baada
ya mechi kuisha,yule refa akiwa njiani kuelekea nyumbani,barabarani akakutana
na taa za kuongozea magari,njano,nyekundu na kijani,ndipo yule refa akapeleka
pendekezo kwa Shirikisho la mchezo wa soka duniani (FIFA),kuwa kutokana na
kutokuelewana kwa lugha ikaamuliwa kutumika kadi mbili,yaani njano na nyekundu
ili kutoa adhabu kwa kadi hizo bila kualibu mchezo.




0 Comments