Ticker

6/recent/ticker-posts

MADOGO WA CARDIFFF CITY WAWACHAKAZA WAKONGWE WA MANCHESTER CITY,WAWACHAPA BAO 3 KWA 2,

Fraizer Campbell alifunga mabao mawili ya Cardiff katika dakika ya 79 na 87 na kusababisha timu yake hiyo iliyo panda daraja msimu huu, kuondoka na pointi tatu muhimu  wakiwa katika uwanja wao wa nyumbani  wa Cardiff City Stadium,na kuwapa ushindi wao wa kwanza msimu huu katika ligi kuu England na kuwaacha wakongwe wa Manchester City wasiamini kilichotokea.
Wanaweza kusonga mbele: Frazier Campbell alifunga mara mbili kwa upande wa Cardif City
Timu hizo zote mbili zilimaliza kipindi cha kwanza zikiwa hazija fungana,lakini katika kipindi cha pili walioanza kushinda walikuwa
ni Manchester city kupitia kwa Edin Dzeko ndani ya dakika ya 52,baada ya kuachia shuti kali lililopita kati kati ya mabeki wawili wa Cardiff City na kupita juu ya mikona ya kipa,na hivyo kuiandikia bao la kwanza Manchester City.
Edin Džeko,alifunga bao kwa kupitIsha mpira kati kati ya wa chezaji wawili wa Cardiff City
Katika dakika ya 60, mchezaji wa Cardiff City Aron Gunnarsson alisawazisha bao hilo na kuufanya ubao kusomeka moja moja,kisha Fraizer Campbell katika dakika ya 79 na 87 akaipatia bao la pili, na la tatu ambalo ndilo la ushindi kwa Cardiff City.
Fraizer Campbell  alifunga katika dakika ya 79 na 87
Aron Gunnarsson,akifunga bao la kwanza la kusawazisha
Shujaa:Fraizer Campbell  inawezekana akaweza kuthibitisha muhimu  wake katika msimu wote,ndani ya  timu hii iliyopanda daraja.
Dakika za mwishoni kabisa yaani katika dakika ya 90, Alvaro Negredo aliipatia bao la pili Manchester City,na huo ndio ukawa mwisho wa mchezo kwani baada ya dakika kadhaa refa alipuliza kipenga kuashilia mpira umekwisha.
Alvaro Negredo akifunga bao la mwisho la Manchester City
Wakati wa kusherehekea: Mashabiki wa Cardiff wakisheherekea bao la  Campbell
Machester City wanakata tamaa
 Shujaa Campbell akiruka juu kushangilia

 Kikosi cha Cardiff City: Marshall 6; Connolly 6, Caulker 7, Turner 7, Taylor 6; Bellamy 6 (Cowie,83mins), Gunnarsson 7, Kim 7 (Mutch, 90mins), Medel 7, Whittingham 6; Campbell 8 (Cornelius, 90mins)
Akiba wasiotumika: Lewis, Hudson, Noone, Maynard
wafungaji: Gunnarsson 60, Campbell 79, 87

Kikosi cha Manchester City: Hart 7; Zabaleta 4, Garcia 4, Lescott 5, Clichy 6; Navas 6 (Nasri, 55mins 5), Fernandinho 6 (Milner, 77mins 5), Toure 6, Silva 7; Aguero 6, Dzeko 7 (Negredo, 69mins 6)
Akiba wasiotumika: Pantilimon, Kolarov, Nastasic,  Rodwell
Wafungaji: Dzeko 52, Negredo 90
Refa: Lee Probert
Jumla ya waliohudhulia: 27, 068

Post a Comment

0 Comments