Ticker

6/recent/ticker-posts

KOMBE LA DUNIA 2014,TIKETI KUANZA KUUZWA

Tiketi kwa ajili ya Kombe la Dunia 2014 nchini Brazil zitaanzwa kuuzwa siku ya  Jumanne,lakini blog  ya Jamii na Michezo inatambua kuwa hata wewe msomaji wa blog hii unao uwezo wakununua tiketi hizo kwa njia  ya tovuti ya FIFA.
 
Tunataka tiketi:picha inaonyesha mashabiki wa Brazil nje ya uwanja wa Maracana
Karibu na tiketi 3.3million zitakuwa zinapatikana kwa ajili ya
mashindano, gharama ni kati ya £ 58 na £ 632 kwa bei ya mwisho katika uwanja wa Maracana mjini Rio.
Kuna mechi 64 katika mashindano na FIFA wana imani kutakuwa na mahitaji sawa na wao katika  Kombe la Dunia la mwaka 2006 nchini Ujerumani.
 
Itajirudia? Wayne Rooney pichani akiipatia bao  timu yake ya taifa la  England dhidi ya Brazil katika uwanja wa Maracana
Maombi tayari  yameshaanza kutumwa katika tovuti ya FIFA,na inasemekena kuwa kuna foleni kutokana na mahitaji kuwa mengi mno kupita kiasi kwa ajili ya kupata tiketi.
 "daima itakuwa ni vigumu kutabiri,"Mkurigenzi wa masoko wa  FIFA  Thierry Weil,aliongea na   BBC.
"Lakini Ninaamini kuwa itakuwa ni zaidi kile kilichotokea katika nchi ya Ujerumani na zaidi ya kilichotokea nchini Afrika Kusini mwaka 2010."


Post a Comment

0 Comments