Gareth
Bale tayari ameshatia nanga nchini Uhispania kujiandaa kusaini katika klabu ya Real Madrid, lakini
Tottenham na viongozi wa Kihispania bado hawajaweka wazi suala la pesa iliyopendekezwa ambayo itavunja rekodi ya dunia.
mchezaji huyo wa kimataifa wa Wales ambaye ana umri wa miaka 24, ameruka kwa ndege binafsi akitokea Malaga na kisha alisafiri kwa teksi mpaka Marbella, ambapo anatarajiwa kukaa na kufanya
Awali Jamii na Michezo tuliripoti kuwa klabu ya Real Madrid imetoa ofa mbili tofauti kawa ajili ya kumchukua winga Gareth Bale na kusuburi kuona klabu ya Tottenham Hotspur inachagua ofa moja,na ofa ya kwanza ambayo ni ya €100m (£ 86m) malipo yatayo
ambatana na mkataba wa miaka mitatu hadi minne,ambayo itakuwa
imeishinda ofa iliyovuka rekodi ya dunia kutoka Manchesta united kwa
Cristian Ronaldo ya £80m.
Na ofa nyingine
ni malipo ambayo itakuwa karibu na £ 70m,ofa hii itakuwa inamfanya kuwa
mchezaji wa ghali sana,kwani itamuwezesha kumfanya kuwa mchezaji anayelipwa
mshahala mkubwa na wenye thamania kuliko Cristian Ronaldo.
![]() |
| Jukwaa la kimataifa:Real Madrid wanaonekana kufanya matayarisho ya jukwaa ndani ya Bernabeu,kwa ajili ya kumkaribisha Gareth Bale |
Real
Madrid inacheza siku ya jumatatu usiku na timu ya Granada katika La Liga,na Bale anatarajiwa kutambulishwa kabla ya Jumanne.



0 Comments