Ticker

6/recent/ticker-posts

Press Conference:Simba SC na AFC Leopards/Viingilio/kuna habari njema/wanasimba wazidi kuchukuwa Fomu

Mhariri:Herman Kihwili. IMEWEKWA 07,SEPT.2018 SAA 12:50 JIONI

Mabingwa wa soka Tanzania bara Wekundu Wa Msimbazi Simba, kesho watacheza mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya AFC Leopard kutoka
nchini Kenya, ikiwa ni sehemu ya kujiandaa na mchezo wa mzunguuko wa tatu wa ligi kuu ya soka Tanzania bara utakaowakutanisha na Ndanda FC mjini Mtwara mwishoni mwa juma lijalo.
Afisa habari na mawasiliano wa klabu ya SImba Haji Sunday Manara amesema mchezo huo utachezwa kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es salaam mishale ya saa kumi na mbili jioni.

Mbali na mchezo huo wa kimataifa wa kirafiki utakaochezwa kesho uwanja wa taifa Dar es salaam, Haji Manara akatumia nafasi ya mkutano na waandishi wa habari kuwakumbusha wanachama wa klabu ya Simba kutumia muda uliopo kuchukua fomu za kuwnaia nafasi mbalimbali za uongozi wa klabu hiyo.
BOFYA CHINI KUSIKILIZA 
...>>>.....

KWA TAARIFA,BREAKING NEWS,RATIBA PAMOJA NA MATOKEO YA MECHI MBALIMBALI,LIKE PAGE YA FACEBOOK  BONYEZA HAPA (Jamii na Michezo),na instagram- kihwiliupdates

Post a Comment

0 Comments