Ticker

6/recent/ticker-posts

VIDEO:Roma Mkatoliki afungiwa miezi 6,Nay wa mitego afunguka

Mhariri:Herman Kihwili. IMEWEKWA.MARCH.01.2018 SAA 11:52 JIONI



BARAZA la Sanaa Tanzania (BASATA) limemfungia Rapa Ibrahim Mussa ‘Roma Mkatoliki’ kwa muda wa miezi sita
kutojihusisha na sanaa ya muziki kutokana na kutotii agizo la Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo lililomtaka kubadilisha maudhui ya wimbo wake wa KIBAMIA.
Kutokana na wimbo huo ambao Roma amewashirikisha wasanii wenzake, Stamina na Maua Sama, Basata walimuita na kumweleza arekebishe maudhui ya wimbo lakini inasemekana hakutekeleza agizo hilo hivyo BASATA wameamua kumfungia.
Maamuzi ya kufungiwa kwa msanii huyo yametangazwa na naibu waziri wa habari, sanaa, utamaduni na michezo Julianza Shoza alipozungumza na waandishi wa habari hii leo jijini Dar es salaam.

Katika hatua nyingine Wiziri wa habari, sanaa, utamaduni na michezo imempa onyo msanii Nay wa Mitego baada ya kufanya naye mazungumzo,ambapo Nay wa Mitego amepewa maelekezo ya kufanya mabadiliko katika moja ya nyimbo zake ambazo zina maneno tata.

Ney Wa Mitego alikufanya mazungumzo na viongozi wa BASATA pamoja na wizara ya habari, usanii na michezo, na kuahidi kufanya marekebisho ya baadhi ya maneno tata katika wimbi wake wa Mikono Juu.


VIDEO

...

KWA TAARIFA,BREAKING NEWS,RATIBA PAMOJA NA MATOKEO YA MECHI MBALIMBALI,LIKE PAGE YA FACEBOOK  BONYEZA HAPA (Jamii na Michezo),na instagram- kihwiliupdates

Post a Comment

0 Comments