Mhariri:Herman Kihwili. IMEWEKWA.SEPT.27,2016 SAA 06:46 MCHANA
Maandalizi ya mchezo wa Simba na Yanga utakaopigwa jumamosi hii katika uewanja wa Taifa Jijini Dar es salaam
yamekamilika,mara baada ya hii leo viongozi wa vilabu hivyo ,Shilikisho la Soka nchiniTff , kampuni ya Selcom kufanya kikao cha pamoja kujadili juu ya mapato yatakayopatikana kuhakikisha yanafika katika sehemu husika .
yamekamilika,mara baada ya hii leo viongozi wa vilabu hivyo ,Shilikisho la Soka nchiniTff , kampuni ya Selcom kufanya kikao cha pamoja kujadili juu ya mapato yatakayopatikana kuhakikisha yanafika katika sehemu husika .
![]() |
| Kushoto ni meneja miradi wa kampuni inayoshughulika na mfumo wa malipo ya kieletroniki ya Selcom Galus Lunyeta akiwa na Afisa habari wa Tff Afred Lucas hii Leo |
Katika kikao hicho pia wamejadili juu ya viingilio
ambapo V.I.P ni shilingi 30,000 V.I.P B
na C 20,000 Mzunguko 7,000,pia mashabiki wataweza kununua kadi kwa shilingi 7,000 tu hiyo hiyo badala ya kutoa shilingi 3,000 ya gharama ya
kadi peke yake ili kuweza kuondoa msongamano kwa mara ya kwanza.
Kuelekea katika mchezo huo Barabara ya chang’ombe itafungwa
lakini kutakuwa na wakala wa kuuza kadi
ili kuondoa msongamano,Barabara nyingine
itakayofungwa ni ya Sigara.
Kadi zitakavyopatikana
katika Vituo vya mafuta vya TOTAL,PUMA na matawi yote ya Samaki Samaki,
na kwa wakala mbalimbali kama Buguruni sheri,Ilala,Sinza,Mlimani City Uwanja wa
Taifa N.K,pia imesisitizwa watu wapate Tiketi mapema ili kuondoa msongamano.



0 Comments