Mhariri:Herman Kihwili. IMEWEKWA.AUG 6,2016 SAA 01:03 USIKU
Uongozi, wanachama na mashabiki wa klabu ya Simba hii leo
wamefanya usafi katika mtaa wa Msimbazi maeneo yanayozunguuko
majengo ya klabu
hiyo kongwe ambayo mwanzoni mwa juma lijalo itakua na inaazimisha miaka 80
tangu kuanzishwa kwake.
Azimio hilo la kufanya usafi ni sehemu ya kukamilisha
shughuli za samba wiki ambazo zilitangazwa na uongozi wa klabu ya Simba kupitai
raisi wake Evance Aveva majuma mawili yaliyopita mbele ya waandishi wa habari.
Makamu wa rais wa klabu ya Simba Geoffrey Nyange Kaburu alishiriki katika zoezi hilo ambalo
lilichukua zaidi ya saa moja, na mara baada ya kukamilishwa kwake, aliwashukuru
wanachama pamoja na mashabiki waliojitokeza.
Naye mbunge wa jimbo la Ilala ambapo ndipo klabu ya Simba
ilipo, Mussa Azzan Zungu alishiriki katika zoezi la kufanya
usafi katika mtaa wa Msimbazi na alipata nafasi ya kuzungumza na wanachama
pamoja na mashabiki walioshiriki katika zoezi hilo.
Zungu alitoa shukurani pamoja na kuwataka viongozi wa
klabu ya Simba kuwa kitu kimoja ili kuhakikisha klabu hiyo inapiga hatua na
kuondoka hapa ilipo sasa.
ANGALIA PICHA
0 Comments